Mazingira : Wamiliki wa Viwanda waliojenga juu ya mitaro ya majitaka kuingia Hatiani -Mpina - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


21 Dec 2016

Mazingira : Wamiliki wa Viwanda waliojenga juu ya mitaro ya majitaka kuingia Hatiani -Mpina


NA EVELYN MKOKOI -DSM

Akiwa katika siku nyingine ya ukaguzi wa mazingira jijini Dar es salaam, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, leo ametembelea katika Maeneo ya keko Magurumbasi na kujionea namna ambavyo wamiliki wa viwanda wanavyotiririsha maji katika mfereji maarufu kwa jina la mseleleko.

Baada ya ukaguzi wa mazingira katika maeneo hayo, Naibu Waziri Mpina amewaasa wawekezaji wenye viwanda nchini waliojenga juu ya miundombinu ya majitaka kutafuta njia nyingine ya ujenzi sahihi ya miundombinu ya majitaka kutoka viwandani mwao kwenda kwenye mfumo wa mamlaka za maji na kuelekeza kuwa iwapo wataonekana kuziba kwa ujenzi wa majengo yao mitaro mikubwa ya miundombinu ya maji, sheria itachukua mkondo wake ikiwa ni pamoja na kubomoa majengo yao.

Akijibu swali la mwandishi wa habari wa kituo kimoja cha television hapa nchini, lilihoji kuusika kwa watumishi wa umma kwa namana moja au nyigine kiujanja ujanja katika kuruhusu vibali vya ujenzi na kupelekea uharibifu wa miundombinu ya majitaka na mazingira kwa ujumla, Mpina alisema kuwa endapo kutagundulika kuwa na ushiriki wowote wa watumishi wa umma katika suala hilo sheria pia itachukua mkono wake.

Pamoja na hilo Naibu Waziri Mpina amewaeleza wenye viwanda wanaoendelea kuchafua mazingira kuwa kutakuwa na oparesheni kubwa nchini ya ukaguzi wa mazingira itakayohusisha halmashauri za miji, mamlaka za maji, wamiliki wa mabomba ya maji taka na wananchi ili kuwajibika kwa pamoja katika kunusuru uharibifu wa mazingira.

Aidha Ameliagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC kuiandikia hati ya zuwio TANROADS ya mwezi mmoja itayowataka wafumue karavati lao linalopita chini ya barabara katika eneo la kurasini BP darajani na kuliongeza ukubwa ili majitaka yaweze kupita kwa nafasi.

Naibu waziri Mpina Pia amewataka Viongozi wa Manispaa ya Ilala kusimamia kikamilifu usafi wa Mazingira na kuwataka wananchi wa eneo la keko magurumbasi wanaokaa karibu na mfereji wa mseleleko kufanya usafi katika mfereji huo na kutooutumia kama DAMPO.

Kwa upande wake mratibu wa Mazingirawa kanda ya mashariki kutoka NEMC Bw. Jaffari Chimgege amesema wao kama Baraza watakaa kwa Pamoja na wawekezaji, wenye makaravati madogo yanazoshindwa kupitisha majitaka vizuri jijini DSM na kutafuta suluhisho la kudumu kwani hali hiyo ni hatari hasa katika kipindi cha mvua, inaweza kusababisha magojwa ya milipuko kama vile kipindupindu.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina, kulia akiwa katika ziara ya ukaguzi wa Mazingira Keko magulumbasi katika mfereji wa maji taka mseleleko Jijini Dar es salaam mara baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi wanaoishi maeneo hayo.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina akimsikiliza Mtaalamu wa Mazingira kutoka NEMC, Jaffar Chimgege katika ziara hiyo ya ukaguzi wa mazingira jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina, akiwa ameongozana na wananchi wanaoishi maeneo ya Keko Magulumbasi katika ziara ya ukaguzi wa Mazingira.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya ukaguzi wa mazingira Keko Jijini Dar es salaam.

Post Top Ad