Matukio : Nape ,Mbowe waongoza kuuaga mwili wa Mpoki Bukuku Dar - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Tuesday, 27 December 2016

demo-image

Matukio : Nape ,Mbowe waongoza kuuaga mwili wa Mpoki Bukuku Dar







01

Wanahabari wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mwandamizi wa The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku baada ya kutolewa heshima za mwisho katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Tabata, Dar es Salaam, tayari kulisafirishwa kwenda kwao Msalato Dodoma kwa mazishi. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

02

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akiwaongoza waombolezaji kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mwandamizi wa The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Tabata, Dar es Salaam. Mwili wa Mpoki ulisafirishwa kwenda kwao Msalato Dodoma kwa mazishi.

03

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa mpendwa wetu Mpoki Bukuku

04

Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa akiwa ameshika shada la maua alipokuwa akiingiza kwenye gari lenye jeneza la mwili wa marehemu Mpoki Bukuku

05

Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo ambaye pia ni Mmiliki wa Blog hii, Richard Mwaikenda akitoa salamu za rambirambi za Chama cha Mabloga Tanzania (TBN) wakati wa kuaga mwili wa mpendwa Mpoki Bukuku.

IMG_3824

Mwakilishi wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Habari Tanzania (MOAT), Saed Kubenea akitoa salamu za rambirambi

IMG_3831

Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akitoa salamu za rambirambi

IMG_3841

Mwakilishi wa Chama cha Wapigapicha za Habar Tanzania (PPAT), Selemani Mpochi akitoa salamu za rambirambi. Mpoki alikuwa mwanachama wa chama hicho.

IMG_3842

ADMIN wa Group la WhatsApp la Tasnia, Thomson Kasenyenda akita salamu za rambirambi na kuahidi group hilo kuwasilisha mchango wao kwa kulipia ada za shule za watoto wa marehemu

IMG_3844

Mwenyekiti wa Chama cha Bongo Movie, Steven Nyerere akitoa salamu

IMG_3870

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo na Burudani Tanzania (TASWA), Juma Pinto akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Mpoki Bukuku.

IMG_3872

Benny Kisaka akitoa heshima za mwisho

IMG_3875

Mhariri Mtendaji wa The Guardian, Mgamba akitoa heshima za mwisho

IMG_3878

Mmiliki wa Blog ya Michuzi, Muhidini Issa Michuzi akitoa heshima za mwisho

IMG_3880

Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao Mpoki Bukuku

IMG_3883




IMG_3891

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete akitoka kutoa heshima za mwisho

IMG_3892




IMG_3894

Mpigapicha wa The Guardian na Nipashe akisaidiwa baada ya kutoa heshima za mwisho

IMG_3906

Mpigapicha wa zamani wa Daily News, Athuman Khamisi akitoa heshima za mwisho

IMG_3908

Mtoto wa kike wa maraehemu Mpoki Bukuku akimvalisha Rozali wakati wa kuaga mwili wa babake

IMG_3913

Mjane wa marehemu Lillian akiubusu mwili wa mumewe

IMG_3914

Mtoto wa kiume wa marehemu Mpoki Bukuku, Junior akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa babake

IMG_3919




IMG_3931

Jeneza lenye mwili wa mpendwa wetu Mpoki Bukuku likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Msalato Dodoma kwa mazishi.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *