Mkuu
wa wilaya ya Kindondoni Mh Aly Hapi akikagua na kujionea bidhaa za
mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Betty Mngulwi mwisho mwa
wiki ambapo Airtel iliwakutanisha baadhi ya wajasiliamali jijini Dar es
salaam katika maonyesho maalum ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’
nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco kwa lengo la kuwakutanisha
wajasiliamali hao na wateja mbalimbali ili kuwatanua masoko yao na kuuza
bidhaa zao. pamoja nae ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi
Beatrice Singano wakwanza kulia.
Mkuu
wa wilaya ya Kindondoni Mh Ally Hapi akipokea zawadi ya keki toka kwa
mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Diana Moshi mwishoni mwa
wiki mara baada ya kutembelea banda la mjasiliamali huyo wakati wa
maonyesho ya bidhaa za wajasiliamali katika maonyesho ya ‘Airtel FURSA
Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco yaliyoandaliwa
na Airtel kwa lengo la kuwakutanisha wajasiliamali hao na wateja wa
airtel ili kuwatanua masoko yao na kuuza bidhaa zao. pamoja nae ni
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano wakwanza kulia.
Mkuu
wa wilaya ya Kindondoni Mh Ally Hapi akiangalia picha ya mapambo ya
Afrika dansi iliyochorwa na mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA
Bi Theresia Mariatabu wakati alipotembelea banda la mjasiliamali huyo
katika maonyesho ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu
ya Airtel Morocco yaliyoandaliwa na Airtel kwa lengo la kuwakutanisha
wajasiliamali hao na wateja wa airtel ili kuwatanua masoko yao na kuuza
bidhaa zao. pamoja nae ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi
Beatrice Singano na mkurugenzi Rasilimali watu wa Airtel Bw, Patrick
Foya kulia.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi Beatrice Singano Mallya akizungumza katika hafla hiyo.
Kampuni
ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa Airtel FURSA mwisho
mwa wiki imewakutanisha baadhi ya wajasiliamali jijini Dar es salaam
katika maonyesho maalum ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’
yaliyoandaliwa nje ya kiwanja cha ofisi kuu ya Airtel vilivyoko Morocco
kwa leongo la kuwakutanisha wajasilimali hao na wateja mbalimbali kwa
lengo la kuwawezesha kutanua masoko yao na kuuza bidhaa zao.
Baadhi
ya wajasiriamali walionufaika na mradi wao wa kijamii wa Airtel FURSA
nao walipata nafasi za kuhudhuria na kuonyesha bidhaa zao huku
wakiipongeza Airtel kwa kuendelea kuwasaidia kuboresha biashara zao.
“Airtel
leo wametusaidia sana sisi kukutana na wajasiliamal wenzetu
tukabadilishana ujuzi pamoja na kubadilishana mawasiliano ili tuweze
kusaidiana kupeana masoko, vilevile hapa katika jengo tumejipatia wateja
wengi sana, hatujaamini kabisa kama tungeweza kuuza hivi, mimi nauza
keki nimepata wateja hata wa baadae, kunawenzangu wanaouza Kuku, Mayai,
Picha za mapambo ya nyumabani, Mito ya mapambo, Ubuyu, Matunda na Sabuni
za kufanyia usafi nyumbani nimefurahi kuona kila mtu ameuza na
amejitengenezea wateja wa baadae” alieleza mnufaika wa Airtel FURSA Bi
Diana Mushi
Tunawashukuru
sana Airtel kwa kutupatia jukwaa hili la kuonyesha bidhaa na huduma
zetu kwa wadau mbalimbali na kutuongezea wigo wa soko letu. Alisisitiza
Bi Diana
Akitembelea
maonyesho hayo mkuu wa wilaya ya kinondoni alieleza kufurahishwa kwake
na vijana hao huku akiwahimiza vijana wengine kuanziasha biashara ndogo
ndogo ili na kuzisimamia vyema ili kutengeneza ajira kwa vijana wengine
wengi nchini
“Nchi
yetu imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi sana ikiwa ni pamoja na
ardhi yenye rutuba, wanyama na rasilimali nyingine nyingi na bado vijana
wengi wanakabiliwa na janga la kukosa ajira ambalo uwiano wa ukosefu
wa ajira kwa vijana unakua kwa kasi kila mwaka. Napenda kuwapongeza sana
vijana mlioamua kujikita kwenye ujasiriamali bila kujali changamoto
zilizoko katika biashara, nawatia moyo vijana wengine kuiga mfano na
kujiajiri wenyewe na kukuza maendeleo ya jamii zetu” alisema Mkuu wa
wilaya ya Kinondoni, Mh Ally Hapi.
Akionge
kuhusu mradi wa Airtel FURSA Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi
Beatrice Singano Mallya alisisitiza dhamira ya kampuni yake kuendelea
kuwawezesha vijana wajasiriamali nchini kwani wanatambua ndio chachu
kubwa ya kuinua maendeleo ya jamii
“Airtel
FURSA imejipanga kuendelea kuwawezesha vijana ka ili kuweza kuzikamata
fursa zitakazowawezesha kufikia ndoto zao kama ilivyofanya leo kupitia
maonyesho haya ya ndani ya biashara ya Airtel FURSA wajasiliamali
Bazaar” alisema Bi Singano
Bi
Singano alimalizia kusema kuwa “Airtel tunaona fahari kwa kufanikiwa
kwa mradi huu ambapo mpaka sasa vijana zaidi ya 5000 wamenufaika na
elimu ya ujasiriamali na kati yao zaidi ya vijana 100 waliopo katika
makundi na binafsi wamewezeshwa kwa kupatiwa vitendea kazi ili kuongeza
uzalisjhaji wenye thamani”.
Mradi
wa Airtel FURSA ulianzishwa mwaka jana mwezi wa tano kwa lengo la
kuwawezesha vijana wajasiriamali kuweza kukuza biashara zao na kuchochea
vijana wengi kujikita kwenye ujasirimali kwa lengo la kuinua uchumi wao
na jamii inayowazunguka, pia mradi umelenga kutoa katika elimu ya
ujasiriamali kwa vijana ili kuwawezesha kujua jinsi ya kuendesha
biashara na namna ya kutatua changamoto za kibiashara na kupata faida
zaidi.
No comments:
Post a Comment