Teknolojia : Airtel FURSA yawafungulia masoko mapya wajasiliamali wadogo wadogo jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


1 Nov 2016

Teknolojia : Airtel FURSA yawafungulia masoko mapya wajasiliamali wadogo wadogo jijini Dar

Mkuu wa wilaya ya Kindondoni Mh Aly Hapi akikagua na kujionea bidhaa za mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Betty Mngulwi mwisho mwa wiki ambapo Airtel iliwakutanisha baadhi ya wajasiliamali jijini Dar es salaam katika maonyesho maalum ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco kwa lengo la kuwakutanisha wajasiliamali hao na wateja mbalimbali ili kuwatanua masoko yao na kuuza bidhaa zao. pamoja nae ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano wakwanza kulia.
Mkuu wa wilaya ya Kindondoni Mh Ally Hapi akipokea zawadi ya keki toka kwa mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Diana Moshi mwishoni mwa wiki mara baada ya kutembelea banda la mjasiliamali huyo wakati wa maonyesho ya bidhaa za wajasiliamali katika maonyesho ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco yaliyoandaliwa na Airtel kwa lengo la kuwakutanisha wajasiliamali hao na wateja wa airtel ili kuwatanua masoko yao na kuuza bidhaa zao. pamoja nae ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano wakwanza kulia.
Mkuu wa wilaya ya Kindondoni Mh Ally Hapi akiangalia picha ya mapambo ya Afrika dansi iliyochorwa na mjasiliamali aliyewezeshwa na Airtel FURSA Bi Theresia Mariatabu wakati alipotembelea banda la mjasiliamali huyo katika maonyesho ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ nje ya ofisi kuu ya Airtel Morocco yaliyoandaliwa na Airtel kwa lengo la kuwakutanisha wajasiliamali hao na wateja wa airtel ili kuwatanua masoko yao na kuuza bidhaa zao. pamoja nae ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano na mkurugenzi Rasilimali watu wa Airtel Bw, Patrick Foya kulia.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi Beatrice Singano Mallya akizungumza katika hafla hiyo.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa Airtel FURSA mwisho mwa wiki imewakutanisha baadhi ya wajasiliamali jijini Dar es salaam katika maonyesho maalum ya ‘Airtel FURSA Wajasiliamali Bazaar’ yaliyoandaliwa nje ya kiwanja cha ofisi kuu ya Airtel vilivyoko Morocco kwa leongo la kuwakutanisha wajasilimali hao na wateja mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha kutanua masoko yao na kuuza bidhaa zao.

Baadhi ya wajasiriamali walionufaika na mradi wao wa kijamii wa Airtel FURSA  nao walipata nafasi za kuhudhuria na kuonyesha bidhaa zao huku wakiipongeza Airtel kwa kuendelea kuwasaidia kuboresha biashara zao.

“Airtel leo wametusaidia sana sisi kukutana na wajasiliamal wenzetu tukabadilishana ujuzi pamoja na kubadilishana mawasiliano ili tuweze kusaidiana kupeana masoko, vilevile hapa katika jengo tumejipatia wateja wengi sana, hatujaamini kabisa kama tungeweza kuuza hivi, mimi nauza keki nimepata wateja hata wa baadae, kunawenzangu wanaouza Kuku, Mayai, Picha za mapambo ya nyumabani, Mito ya mapambo, Ubuyu, Matunda na Sabuni za kufanyia usafi nyumbani nimefurahi kuona kila mtu ameuza na amejitengenezea wateja wa baadae” alieleza mnufaika wa Airtel FURSA Bi Diana Mushi

Tunawashukuru sana Airtel kwa kutupatia jukwaa hili la kuonyesha bidhaa na huduma zetu kwa wadau mbalimbali na kutuongezea wigo wa soko letu. Alisisitiza Bi Diana

Akitembelea maonyesho hayo  mkuu wa wilaya ya kinondoni alieleza kufurahishwa kwake na vijana hao huku akiwahimiza vijana wengine kuanziasha biashara ndogo ndogo ili na kuzisimamia vyema ili kutengeneza ajira kwa vijana wengine wengi nchini 

“Nchi yetu imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi sana ikiwa ni pamoja na ardhi yenye rutuba, wanyama na rasilimali nyingine nyingi na bado vijana wengi wanakabiliwa na janga la kukosa ajira ambalo uwiano  wa ukosefu wa ajira kwa vijana unakua kwa kasi kila mwaka. Napenda kuwapongeza sana vijana mlioamua kujikita kwenye ujasiriamali bila kujali changamoto zilizoko katika biashara, nawatia moyo vijana wengine kuiga mfano na kujiajiri wenyewe na kukuza maendeleo ya jamii zetu” alisema Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Mh Ally Hapi.

Akionge kuhusu mradi wa  Airtel FURSA Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi Beatrice Singano Mallya  alisisitiza  dhamira ya kampuni yake  kuendelea kuwawezesha vijana wajasiriamali nchini kwani wanatambua ndio chachu kubwa ya kuinua maendeleo ya jamii

“Airtel FURSA imejipanga kuendelea kuwawezesha vijana ka ili kuweza kuzikamata fursa zitakazowawezesha kufikia ndoto zao kama ilivyofanya leo kupitia maonyesho haya  ya ndani ya biashara  ya Airtel FURSA wajasiliamali Bazaar” alisema Bi Singano

Bi Singano alimalizia kusema kuwa “Airtel tunaona fahari kwa kufanikiwa kwa mradi huu ambapo mpaka sasa vijana zaidi ya 5000 wamenufaika na elimu ya ujasiriamali na kati yao zaidi ya vijana 100 waliopo katika makundi na binafsi wamewezeshwa kwa kupatiwa vitendea kazi ili kuongeza uzalisjhaji wenye thamani”.

Mradi wa Airtel FURSA ulianzishwa mwaka jana mwezi wa tano kwa lengo la kuwawezesha vijana wajasiriamali kuweza kukuza biashara zao na kuchochea vijana wengi kujikita kwenye ujasirimali kwa lengo la kuinua uchumi wao na jamii inayowazunguka, pia mradi umelenga kutoa katika elimu ya ujasiriamali kwa vijana ili kuwawezesha kujua jinsi ya kuendesha biashara na namna ya kutatua changamoto za kibiashara na kupata faida zaidi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad