Matukio : Rais Dk. Magufuli afungua barabara ya Nairobi Southern Bypass katika eneo la Karen nchini Kenya - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


1 Nov 2016

Matukio : Rais Dk. Magufuli afungua barabara ya Nairobi Southern Bypass katika eneo la Karen nchini Kenya


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Naibu Rais wa Kenya William Rutto pamoja na viongozi wengine, wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya kupunguza msongamano ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kuwasili katika eneo ka Karen jijini Nairobi kwa ajili ya kufungua rasmi barabara ya kupunguza msongamano ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati wa nyimbo za Taifa zikipigwa mara baada ya kuwasili katika eneo la Karen jijini Nairobi.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Karen nchini Kenya mara baada ya kufungua barabara ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.



Sehemu ya barabara hiyo ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakicheza wimbo pamoja na kikundi cha kwaya katika eneo la Karen mara baada ya kufungua barabara hiyo ya Nairobi Southern Bypass nchini Kenya.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Bi. Lucy Karuga kuhusu usindikaji wa mazao ya chakula katika kiwanda cha Maziwa cha Eldoville katika eneo la Karen nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia usindikaji wa Samli katika kiwanda hicho cha maziwa cha Eldoville nchini Kenya.PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad