Uchumi : Wamisri watangaziwa Fursa za uwekezaji hapa nchini - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Oct 2016

Uchumi : Wamisri watangaziwa Fursa za uwekezaji hapa nchini

Mhe. Mohammed Haji Hamza, Balozi wa Tanzania nchini Misri akiwakaribisha wageni waliohudhuria katika ufunguzi wa kongamano la biashara kati ya Tanzania na misri lililofanyika katika miji ya Cairo na Alexandria kuanzia tarehe 17 hadi 19 Oktoba 2016. Kongamano hili lililowakutanisha wafanyabiashara kutoka nchi hizi mbili lilifunguliwa na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Zanzibar, Mhe Balozi Amina Salim Ali. 

Kongamano hilo lilihudhuriwa na washiriki kutoka sekta mbalimbali zinahusika na uwekezaji, biashara, ujenzi, usafirishaji, elimu, afya, viwanda, uhandisi ,kilimo na utalii. Kongano hilo liligharmiwa na kuratibiwa kwa ushirikiano kati ya Ubalozi wa Tanzania nchini Misri, Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri, Jumuiya za Wafanyabiashara wa Misri na makampuni binafsi ya biashara ya Misri. Katika kongamano hilo washiriki wa Tanzania pamoja na kutoa mada zilizohusu fursa za biashara na uwekezaji nchini Tanzania na hasa katika sekta ya viwanda na utalii pia walipata fursa ya kushiriki katika mazungumzo ya ana kwa ana ya kibiashara.

Siku ya pili ya kongamano hili washiriki kutoka Tanzania walipata nafasi ya kutembelea sehemu mbalimbali za uzalishaji na huduma zikiwemo: kijiji cha teknolojia cha Cairo, viwanda vya utengezaji madawa, vifaa tiba na rangi za ujenzi mjini Cairo pamoja na viwanda vya nguo, vifaa vya ujezi na samani za chuma katika miji wa Tenth Ramadhani . 

 Siku ya tatu ya kongamano hilo baadhi ya washiriki kutoka Tanzania walitembelea vyuo vikuu vya Alexandria na chuo kikuu cha kiarabu cha sayansi, teknolojia na usafiri wa bahari mjini Alexandria na kuwa na mazungumzo ya ushirikiano na viongozi wa vyuo vikuu hivyo. 

Ujumbe wa Tanzania pia ulipata nafasi ya kutembelea kiwanda cha kutengenezea manukato kilichopo nje kidogo ya jiji la Akexandria. Akiwa jijini Cairo, Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika kongamano hilo alipata nafasi ya kukutana na Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Misri, Rais na Mtendaji Mkuu wa Afri exim bank na Katibu Mkuu wa Wakala wa Ushirikiano na Maendeleo wa Misri.
Vingozi mbalimbali walioshiriki kwenye ufunguzi wa konganano la kibiashara mjini Cairo siku ya tarehe 17 Oktoba 2016 wakisimama wakati wa Nyimbo za Taifa za Tanzania na Misri zilipopigwa. Wa kwanza kutokea kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda wa Misri. Wa pili ni Katibu Mkuu wa Wakala wa Ushirikiano na Maendeleo wa Misri, watatu ni Mhe Balozi Amina Salim Ali, Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Zanzibar, akifuatiwa na Balozi wa Tanzania nchini Misri, Mhe. Mohamed Haji Hamza , watano ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar na wa sita ni Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Biashara ya Misri. Waliosimama mbele ya meza kuu ni Mabalozi kutoka nchi za SADC waliopo mjini Cairo. 
Balozi Amina Salum Ali, Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko wa Zanzibar akifuatilia neno la ukaribisho kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Misri, Mhe. Mohammed Haji Hamza .
Balozi Hamza akisalimiana na kubadilishana mawazo na washiriki mbalimbali wa kongamano la biashara jijini Cairo mara baada ya ufunguzi kukamilika.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad