Muziki : YCEE aungana na Dj Maphorisa wa Afrika Kusini kwenye Remix ya OMO ALHAJI - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


10 Oct 2016

Muziki : YCEE aungana na Dj Maphorisa wa Afrika Kusini kwenye Remix ya OMO ALHAJI




Msanii wa Hip-hop wa Nigeria, Ycee ameungana na mtayarishaji wa muziki na muimbaji wa Afrika Kusini, DJ Maphorisa kwenye remix ya wimbo wake unaofanya vizuri barani, ‘Omo Alhaji’.

Ikifanyika jijini Johannesburg, na kuongozwa na La Dupont Productions, remix ya wimbo huo inahusisha rap iliyoshiba na inayohitaji usikivu.

DJ Maphorisa amechanganya ladha ya kipekee ya Kusini kwenye mrindimo unaoungana vyema na mtindo wa Ycee na kuzalisha wimbo utakaofanya vizuri kwenye klabu, mtaani na hata kwenye redio. Remix hii ya Omo Alhaji, haina shaka itateka tena mawimbi ya redio na TV barani Afrika.

Ycee anasema, “Limekuwa jambo kubwa kufanya remix hii, kama msanii ninafurahi kujaribu muziki tofauti. Ulikuwa uzoefu mkubwa na wa kufurahia kufanya kazi na DJ Maphorisa. Ninaamini mashabiki watafurahia remix hii.”

KUHUSU YCEE

Akizaliwa kwa jina la Alejo Martin Oludemilade, tarehe 29, January 1993, Ycee ni msanii wa hip hop wa Nigeria na mshindi wa tuzo.  Amesainishwa kwenye lebo ya muziki ya TINNY ENTERTAINMENT. Alianza rasmi muziki Disemba 2012 kwa kuachia wimbo 'Smile on Me' uliotayarishwa na Jay Sleek, na zingine kama 'Pass Me' na 'Amen' akimshirikisha Mbryo.

Alikuja kujipatia umaarufu zaidi July 2015 baada ya kuachia wimbo 'Jagaban.' Jagaban ukaja kuwa miongoni mwa nyimbo kubwa zaidi kwa mwaka 2015/16 na kuja kuwa na remix nzito aliyomshirikisha staa wa YBNL, Olamide na video yake ikiongozwa na Director Q.

Wimbo huo ulimweka sehemu nzuri Ycee kama kinara wa hip hop ya kizazi kipya nchini Nigeria na hatimaye kumpa tuzo ya “Rookie Of The Year” kwenye tuzo za Headies, mwaka 2015.

Kutoka kwa wimbo ‘Omo Alhaji’, Disemba 2015, kulimpandisha zaidi Ycee kama mmoja wa wasanii wakali kabisa wa hip hop nchini Nigeria. Alikuja kuachia video ya wimbo huo iliyoongozwa na Director Q iliyofanyika Uingereza. Wimbo huo pamoja na video yake viligeuka wimbo wa taifa kwenye chati za redio za TV za Nigeria, kwenye klabu na hata mtaani huku ukiipa umaarufu sentesi: 'Who's your Daddy?

EP yake ya kwanza iliyopewa jina The First Wave itatoka Oktoba, 2016.

KUTAZAMA VIDEO HIYO FUATA LINK HIYO CHINI:


MITANDAO YA KIJAMII



KWA BOOKINGS/MAWASILIANO NA UONGOZI
Contact:  +234 812 907 0990





Contact

Salha S Kibwana

 Tele

+255 655 121 421

 


Email

Info@lasconsultancy.co.tz

Website

http://www.lasconsultancy.co.tz

FOR IMMEDIATE RELEASE

10th October, 2016


VIDEO : NIGERIAN HIT MAKER “ YCEE”  TEAMS UP WITH MULTI-TALENTED DJ MAPHORISA FROM SOUTH AFRICA ON THE NUMBER 1 HIT SONG OMO ALHAJI REMIX.
Nigerian Hip-hop hitmaker Ycee teams up with South Africa’s DJ Maphorisa on the remix to his hit song ‘Omo Alhaji’. Shot in Johannesburg, by La Dupont productions, the fast paced remix features Ycee with an energetic flow that commands attention. DJ Maphorisa fuses his unique Southern sound into a rhythm that seamlessly blends with Ycee’s style delivering a sure club, street and radio banger.
This solid Omo Alhaji remix will definitely take over the continent airwaves.  Hip hop artist said  “It was great working on the remix as an artist i enjoy experimenting on a different sound. It was also a great and fun experience working with the talented DJ Maphorisa,I believe the fans will definitely enjoy the remix”

ABOUT YCEE :
Born Alejo Martin Oludemilade on the 29th of January 1993, Ycee is an award winning hip hop artist from Nigeria. He is signed to Nigerian Record Label; TINNY ENTERTAINMENT.His music career kicked off in December 2012 with the release of his first official single 'Smile on Me' produced by Jay Sleek, other singles, 'Pass Me' and 'Amen' featuring Mbryo . He finally gained critical and commercial acclaim in July 2015 with the release of the runaway hit 'Jagaban' 'Jagaban' went on to become one of 2015/16's biggest songs and with an even bigger remix featuring YBNL's Olamide with stellar visuals from Director Q. This further solidified YCEE's position as the leader of Nigeria's new school of Hip Hop and netted him the coveted “Rookie Of The Year” award at the 2015 Headies.
The release of "Omo Alhaji" December 2015 sealed his status as one of Nigeria's biggest hip hop acts. He followed this up with a video also directed by Director Q and shot in the UK. The song and its video rode away to the top of Nigeria's charts, clubs and the streets popularizing the phrase 'Who's your Daddy?
His debut EP, “the first wave” will be released in October 2016
TO WATCH THE VIDEO FIND LINK BELOW;

SOCIAL MEDIA
www.instagram.com/tinnyentafrica
FOR BOOKINGS/MANAGEMENT CONTACT:
Contact:  +234 812 907 0990

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad