Matukio : Muswada wa Habari utatoa fursa kwa chombo cha habari kuomba radhi pasipo kuchukuliwa Hatua na Mamlaka Zinazohusika - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


27 Oct 2016

Matukio : Muswada wa Habari utatoa fursa kwa chombo cha habari kuomba radhi pasipo kuchukuliwa Hatua na Mamlaka Zinazohusika

Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akifanya mahojiano ya kipindi maalum cha heloo Tanzania kinachorushwa hewani na kituo cha redio Uhuru FM cha Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini humo. Kushoto ni mtangazaji wa kipindi hicho, Sheila Simba.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akibadilishana mawazo na Mtangazaji wa kipindi cha heloo Tanzania kinachorushwa hewani na kituo cha redio cha Uhuru FM, Sheila Simba wakati wa ziara ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini humo leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akibadlishana mawazo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Redio Uhuru FM cha Jijini Dar es Salaam, Angel Akilimali ikiwa ni sehemu ya mwendelezo ya ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas (katikati) akizungumza na wahariri na waandishi wa gazeti la Uhuru wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mhariri Mtendaji wa Gazeti hilo, Ramdhani Mkoma na kulia ni Afisa Habari Mwandamizi wa Idara Habari( MAELEZO), Jonas Kamaleki.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akimsalimu mwandishi mwandamizi wa habari za michezo wa gazeti la uhuru, Sophia Ashery wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akimsalimu mwandishi mwandamizi wa gazeti la uhuru, Njumai Ngota wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mhariri Mtendaji wa gazeti la Uhuru, Ramadhani Mkoma akimpatia maelezo kuhusu uhifadhi wa magazeti ya zamani kwa Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wahariri wa Gazeti la Uhuru wakifuatilia kwa makini mkutano wa mazungumzo baina yao na Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas wakati wa ziara yake ya kutembelea ofisi za gazeti hilo leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akizungumza wakati wa mkutano wake na bodi ya uhariri wa gazeti la uhuru wakati wa ziara yake ya kutembela ofisi za gazeti hilo leo Jijini Dar es Salaam. Wengine kutoka kushoto ni Mhariri wa Picha, Yassin Kayombo na Mhariri wa Habari Abdallah Kimweri.
Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas akisalamiana na Mhariri msanifu kurasa wa gazeti la Uhuru, Jane Mihanji mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na Bodi ya Uhariri ya gazeti hilo leo Jijini Dar es Salaam.

………………………………………..

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO.

Dar es Salaam.

SERIKALI imesema muswada wa sheria ya huduma ya habari utatoa fursa kwa vyombo vya habari kuiomba radhi jamii radhi kwa jamii pindi wanapoandika habari zenye upotoshaji na hawatochukuliwa hatua za kisheria kutoka katika mamlaka zinazohusika.

Akizungumza katika mwendelezo wa ziara yake katika vyombo vya habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari, Hassan Abbas alisema hakuna haja ya waandishi wa habari kuuhofia muswada huo kipengele na badala yake wausome na kuelewa na kisha watoe maoni yao ili kuuboresha zaidi.

“Sifa moja ya taaluma ya habari ni kufuata maadili hivyo muswada umetoa fursa kwa mwanahabari kukanusha na kueleza ulichokosea hivyo mwandishi hatashtakiwa endepo akiona amekosea na kusahihisha ikiwemo kuomba radhi” alifafanua Mkurugenzi Abbas.

Kwa mujibu wa Abbas alisema kutakuwa na bodi maalumu itakayosimamia masuala ya maadili kwa waandishi wa habari nchini na hivyo kutoa fursa kwa waandishi hao kuhojiwa na kutoa ufafanuzi wa jambo husika.

Aidha Abbas alisema kuwa ipo misingi ya haki ya habari iliyoanishwa katika mikataba ya kimataifa ikiwemo kifungu cha 19 cha mkataba wa geneva wa mwaka 1966 umeeleza kuhusu haki ya kupata habari na taarifa ingawa upo ukomo katika masuala kadhaa ikiwemo suala la usalama wa taifa.

Aidha Abbas aliongeza kuwa muswada huo umelenga kulinda maslahi na usalama wa wanahabari kwani unazungumzia hali halisi ya mwandishi wa habari ukilinganisha na Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 inayozungumzia haki ya chombo cha habari pekee.

Mkurugenzi Abbas alisema kila taaluma duniani ina bodi yake hivyo imefika wakati kwa Tanzania napo kuwa na bodi ya wanahabari ili kuweza kuitendea haki taaluma ya habari.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad