Matukio :Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Atembelea kiwanda cha Nyama na Stendi ya Msamvu, Morogoro - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


3 Aug 2016

Matukio :Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Atembelea kiwanda cha Nyama na Stendi ya Msamvu, Morogoro

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakizingumza na Mkurugenzi na mshauri wa kiwanda cha nyama cha Ngulu Hills Ranch cha Morogoro , Dunstan Mrutu (kulia kwa Waziri mkuu) )  wakati walipokitembelea kiwanda hicho Agosti 3, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe  Mary wakiteremka kuelekea eneo la kuchinjia ng'ombe katika kiwanda cha nyama Ngulu Hills Ranch kilichopo Morogoro wakati walipokitembelea kiwanda hicho Agosti 3, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kulia) wakikagua eneo la kuchinjia ng'ombe katika kiwanda cha nyama cha Nguru Hills Ranch cha Morogoro  Agosti 3, 2016.  Kushoto ni Mkurugenzi na Mshauri wa Kiwanda hicho, Danstan Mrutu.
 
Watoto na wananchi wa kijiji cha Majichumvi  wilayani Mvomero wakionyesha mabango wakati WaziriMkuu,Kassim Majaliwa aliposimama kijijini kwao kuwasikiliza Agosti 3, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary  (kulia) wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pesheni wa LAPF, Eliud Sanga wakati alipokagua ujenzi wa stendi  mpya ya Msamvu Morogoro Agosti 3, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa Mjini  Morogoro baada ya kukagua ujenzi wa stendi mpya ya Msamvu Agosti 3, 2016. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt.Stephene Kebwe na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF,Eliud Sanga.
 Awamu ya kwanza ya jengo la stendi mpya ya mabasi ya Msamvu mjini Morogoro iliyokamilika kwa asilimia 90. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliitembelea stendi hiyo na kuzungumza na wadau Agosti 3, 2016.
 Waziri mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Bibi Halima Mwishehe alipouliza swali wakati Waziri Mkuu alipozungumza na Wananchi kwenye stendi mpya ya Msamvu Morogoro baada ya kukagua ujenzi wake Agosti 3, 2016.  Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dkt. Stephene Kebwe. 
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad