Matukio : Mhe. Sophia Mjema akabidhiwa msaada wa Madawati - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Wednesday, 3 August 2016

demo-image

Matukio : Mhe. Sophia Mjema akabidhiwa msaada wa Madawati




OTH_0365
Muwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania,Gou Haodong akimkabidhi moja ya dawati kati ya 100 yaliyotolewa na Wafanyabiashara wa Karikoo wenye asili ya China ,kwa Mkuu wa Wa Wilaya ya Ilala,Mh Sophia Mjema mapema leo jijini Dar.
OTH_0323
Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Mh Sophia Mjema akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhiwa madawati 200 kutoka kwa Wafanyabiashara wa Kariakoo wenye asili ya China leo jijini Dar,kwa ajili ya shule ya msingi Maghorofani iliyopo Gongolamboto,jijini Dar Es Salaam.Wafanyabiashara hao waliahidi kumkabidhi Mh.DC Mjema Madawati 200 lakini leo wamekabidhi nusu ya madawati hayo (100),huku mengine yakiendelea kutengenezwa.Shule hiyo ya Maghorofani ilikuwa na uhitaji wa madawati 525,yakapatikana madawati 250 na kupungukiwa madawati 275.
OTH_0304
Muwakilishi wa Balozi wa China nchini Tanzania,Gou Haodong akizungumza kwa ufupi mbele ya Waalimu,wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani),kabla ya kukabidhi madawati 100 yaliyotolewa na Wafanyabiashara wa Kariako wenye asili ya China jijini Dar,pichani kulia ni Mkuu wa Wa Wilaya ya Ilala,Mh Sophia Mjema. 
OTH_0331
Baadhi ya Wanafunzi wa shule hiyo ya Maghorofani wakiwa wamekalia baadhi ya madawati yaliyotolewa na Wafanyabiashara wa Kariakoo wenye asili ya China jijini Dar. 
OTH_0406
Wakiwa katika picha ya pamoja .PICHA NA MICHUZI JR.

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *