Mwezi Mtukufu : Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an Zanzibar Masjid Loota Kiembesamaki Zanzibar. - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Wednesday, 15 June 2016

demo-image

Mwezi Mtukufu : Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an Zanzibar Masjid Loota Kiembesamaki Zanzibar.


 DSC_5091
Mgeni rasmin katika Uzinduzi wa Mashindano ya Kitaifa ya Kuhifadhi Qura-an Zanzibar yalioandaliwa na Jumuiya ya Kihifadhi Quran Zanzibar Naibu Kadhi Mkuu Zanzibar Shekh.Hassan Othma Ngwali(katikati) Amiri wa Jumuiya ya  Kuhifadhi Quran Zanzibar Mwalim Suleiman Omar Naimi Amiri Kuhifadhisha Quran Zanzibar Shekh. Mohammed Alawi Ally, wakifuatilia mashindano hayo yaliowashirikisha Wanafunzi wa Vyuo vya Quran Zanzibar,Tanga Pwani na Morogoro. 
DSC_5093
Viongozi wa Jumuiya ya Kuhifadhisha Qur-an Zanzibar wakifuatilia mashindano hayo yanayofanyika katika Masjid Loota Kiembesamaki Zanzibar na kuwashirikisha Vijana wa Umri mbali. 
DSC_5096
Viongozi wa Kamati ya Kuhifadhi Qur-an  wakiwa katikac Masjid Loota Kiembesamaki wakifuatilia Wanafunzi wakisoma Qur-an wakati wa mashindano hayo yalioandaliwa na Jumuiya ya Kuhifadhisha Qur-an Zanzibar.
DSC_5094
Washiriki wa Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an Zanzibar wakiwa katika Masjid Loota wakisubiri zamu zao kushiriki mashindano hayo. yanayoshindanisha Wahifadhi Qur-an Juzuu 5.10,20 na 25.
DSC_5098
Waumini wa Dini ya Kiislam Zanzibar wakifuatilia mashindano ya kuhifadhi Qur-an yanayofanyika katika Masjid Loota Kiembesamaki Unguja Wilaya ya Magharibi B Unguja.
DSC_5100
Majaji wa Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an Zanzibar wakiwa makini kufuatilia usomani wa Wanafunzi hao katika mashindano hayo. 
DSC_5102
Watoa Aya za Qur-an kwa Washiriki wa Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an Zanzibar wakitoa Aya kwa Washiriki hao.
DSC_5090
Mshinriki wa Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an Juzuu 10 kutoka Zanzibar Mwanafunzi Khayyam Mohammed mwenye umri wa miaka 13. akisoma Qur-an wakati wa mashindano hayo yanayofanyika katika Masjid Loota Kiembesamaki leo 14/6/2016.
DSC_5099
Mwanafunzi kutoka Zanzibar Mussa Hamad mwenye umri wa miaka 9 akishiriki katika mashindano hayo ya kuhifadhi Juzuu 10, yanayofanyika katika Masjid Loota kiembesamaki Unguja 
DSC_5106
Mshiriki wa Mashindano ya Kuhifadhi Qur-an kutoka Zanzibar Mwanafunzi Shakir Hamad Juma. akisoma Qur-an katika mashindano hayo yalioandaliwa na Jumuiya ya Kuhifadhi Qur-an Zanzibar. yaliowashirikisha Wanafunzi 27 Kutoka Zanzibar, Tanga, Pwani na Morogoro.

Imetayarishwa na Mtandao wa Zanzinews.com.
Email othmanmaulid@gmail.com - Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *