Matukio : Madiwani 24 wafikishwa Mahakamani, Arumeru ,Arusha - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


8 Jun 2016

Matukio : Madiwani 24 wafikishwa Mahakamani, Arumeru ,Arusha

Madiwani 24 wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi  Arusha wakisubiri kusomewa shitaka la kuharibu uzio wa eneo la Indumi Makere uzio wenye thamani ya shilingi milioni 7 .Kufuatia mgogoro juu ya umiliki wa shamba hilo lililokua likimilikiwa na halmashauri,Kesi ya madiwani hao itatajwa tena Juni 28 mwaka huu.Picha na Ferdinand Shayo


Na Ferdinand Shayo wa Wazalendo 25 Blog,Arusha.

Madiwani 24 wa Halmashauri ya Wilaya Ya Meru wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi iliyoko jijini Arusha na kusomewa mashtaka ya kuharibu uzio wenye thamani ya shilingi milioni 7 kwenye eneo linalomilikiwa na  Itandumi Makere.
     
Madiwani hao waliofikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Agustine Rwizeli wamekana mashtaka hayo na kudai kutohusika na kitendo hicho.

Wakili wa Anayewawakilisha madiwani hao Charles Abraham amesema kuwa kesi hiyo itatajwa tena juni 28 mwaka huu katika Mahakama hiyo.

Wakati huo huo Mahakama hiyo imetoa hukumu kwa aliyekua akituhumiwa kumkashifu Rais John Pombe Magufuli kwa kutumia mtandao wa Facebook  ,Izack Habakuki mwenye umri wa miaka 40,ambapo baada ya kupatikana na hatia hukumu imetolewa na ameamuriwa kulipa kiasi cha shilingi milioni 7 kama adhabu na iwapo atashindwa kulipa atatumikia kifungo cha miaka 3 jela kwa mujibu wa sheria ya mtandao ya mwaka 2015 kifungu cha 6.

Wakili wa TCRA Johaness Karungura amewataka Watanzania kujihadhari na matumizi mabaya ya mitandao ambayo yanaweza kuwaingiza katika matatizo hivyo kuitumia mitandao hiyo kwa manufaa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad