Afya Zetu : Katibu mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi afanya ziara katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa kinondoni, Jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


26 May 2016

Afya Zetu : Katibu mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi afanya ziara katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa kinondoni, Jijini Dar


Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando (kushoto), akitoa taarifa fupi kabla ya kumribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (katikati), wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni ya Mwananyamala Dar es Salaam leo mchana. Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto, Michael John, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Ali Hapi.
Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Kijazi.
Mkutano ukiendelea.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Makani ya Pentekosti (MMPT), Askofu Saldonie Sinde (katikati), akimkabidhi Katibu Mkuu magodoro 50 yaliyotolewa na Umoja wa Makanisa hayo kwa ajili ya kusaidia hospitali hiyo.



Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Kijazi (katikati), akienda kutembelea hospitali hiyo. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magembe.



Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (kulia), akiwajulia hali wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni ya Mwananyamala alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja katika hospitali hiyo.
Katibu Mkuu Kiongozi akizungumza na viongozi mbalimbali katika ziara hiyo.
Hapa Katibu Mkuu Kiongozi akisikiliza malalamiko kutoka kwa wananchi waliofika katika hospitali hiyo kupata huduma (hawapo pichani)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad