Siasa : Mhe. Lekule Laizer awaonya wanachama wa CCM wasio na msimamo - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Thursday, 14 April 2016

demo-image

Siasa : Mhe. Lekule Laizer awaonya wanachama wa CCM wasio na msimamo



12998579_1207310429301905_1241326064591770242_n
 Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha Lekule Laizer akiwa anaongea na wananchi wa tawi la chama cha mapinduzi Simba lililopo ndani ya kata ya Mbulumbulu
13015242_1207310129301935_4630279774363305930_n
 Katibu wa itikadi na uenezi wa mkoa wa Arusha Shabani Mdoe akiwa anaongea na wananchi wa kata ya mbulumbulu wakati wa ziara ya viongozi wa mkoa wa chama cha mapinduzi
12985437_1207310189301929_8003554613199832798_n

12993539_1207310329301915_4021524090861750899_n


12961516_1207310079301940_6675531304344926280_n


12985437_1207310189301929_8003554613199832798_n
 Katibu wa itikadi na uenezi wa mkoa wa Arusha Shabani Mdoe akiwa anaongea na wananchi wa kata ya mbulumbulu wakati wa ziara ya viongozi wa mkoa wa chama cha mapinduzi


13012892_1207310005968614_8059376291243721551_n
 Katibu  wa ccm wialaya ya karatu Loth Olelemeiruti akiwa anaongea na wananchi
12985535_1207310275968587_3821631109216718876_n
 mmoja wa wananchi wa kata ya mbulumbulu akiwa anamueleza mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha matatizo  yanayowakabili katika kata yao ikiwemo  ukosefu wa barabara
12991080_1207310359301912_8383631414155098660_n


 Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha Lekule Laizer akiwa na baadhi ya viongozi wa matawi wa ccm wa kata ya mbulumbulu  wilayani karatu mkoani Arusha

Na  Woinde Shizza,Karatu

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha Lekule  Laizer amewaagiza viongozi wa  matawi  wa kata ya mbulumbulu na wilaya ya karatu kwa ujumla  kufanya tadhimini ya uchaguzi uliopita haraka iwezekanavyo na kupeleka majibu  kwa katibu wa chama cha hicho wilaya ya karatu  Loth Olelemeiruti  ili kuweza kujua ni watu gani ambao waliweza kuhujumu chama na kuchukuliwa hatua kali.



Hayo aliyasema jana  wakati alipokuwa akiongea na wanachama wa chama cha mapinduzi  ndani ya kijiji  cha Losteti  kilichopo ndani ya kata ya mbulumbulu wilayani Karatu Mkoani Arusha  .



Alisema kuwa katika uchaguziwa uliopita baadhi ya viongozi pamoja na wananchama waliweza kusaliti chama kwa kutoa siri za chama pamoja na kuwapa ushirikiano viongozi wa upinzani hali ambayo ilichangia kwa kiasi kikubwa kupoteza baadhi ya kata.



“napenda kuwaambia viongozi wote wa matawi wafanye tadhimini haraka iwezekanavyo baada ya hapo wapeleke majibu kwa katibu wa wilaya ya karatu ili aweze kuyafikisha mkoani na sisi tuweze kuyatumbua majipu yote ambayo   walikisaliti chama wakati wa kampeni”alisema Laizer



Aidha aliongeza kuwa sasa ivi viongozi wa chama wanatakiwa kufanya kazi kama kwa nguvu zao zote pamoja na akili zao zote ili kuhakikisha chama kinarudi katika mstaari wake na sio hivyo tu iwapo viongozi watafanya kazi kwa nguvu zao zote itasaidia pia kumpa nguvu rais wa nchi ambaye ametoka katika chama cha mapinduzi.



“tunajua watu wengi walichukuliwa na mafuriko sasa napenda kusema yale mafuriko yameisha sasaivi ni kazi tu ,na pia napenda kutumia fursa hii kuwaambia wananchi yeyote ambaye anataka kuwa mwana chama wa ccm achukuwe kadi mapema kwani itafikia mahali chama akitatoa kadi tena na sio kuchukuwa kadi tu bali kulipia ada maaana mwanachama ambaye ajalipa ada ya uanachama basi yeye sio mwananchama hai kwakua ajalipa ada ni bei ndogo sana kwa iyo kila mwanachama anatakiwa alipe ada ili awe mwanachama hai”alisema Laizer

Alibainisha kuwa kwa sasa amana kiongozi ambaye atachaguliwa kwa kutegemea rushwa hivyo ,kama kunamwananchi au mwanachama ambaye anategemea aje achukuwe fomu katika chaguzi zijazo kwa kutoa rushwa au anategemea atatumia pesa zake kushinda katika uchaguzi asahau kabisa maana sasa ivi ndani ya ccm awataki watu ambao wanatumia fedha kupat a nafasi za uongozi  wamepotea kwani aita kubalika kabisa.

Hata  hivyo mwenyekiti huyo amejinasibu kuwa aliyekuwa mgombea wa urais kupitia umoja wa vyama vinavyounda ukawa  Edwad lowasa kamwe atakaa aje kuwa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kulingana na mazambi yake  aliyoyafanya  kwani amefanya nae kazi kwa muda mrefu na anafahamu vizuri.

Kw aupande wake katibu wa itikadi na uenezi mkoa wa Arusha Shabani Mdoe amesema kuwa wao kama viongozi wa chama wamejitoa sadaka kwa ajili ya kuimarisha chama cha mapinduzi  mkoa wa Arusha na watafanya kila jitiada kuhakikisha chama kina simama imara na iwapo kunamtu ndani ya chama anaejijua kuwa ni jipu aanze kujitumbua mapema kabla ajatumbuliwa .

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *