Matukio : RC Makonda amwapisha mkuu wa wilaya mpya wa kinondoni Ally Salum Hapi, Jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


21 Apr 2016

Matukio : RC Makonda amwapisha mkuu wa wilaya mpya wa kinondoni Ally Salum Hapi, Jijini Dar



Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando, akizungumza wakati akielezea kuhusu hafla ya kumwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (wa pili kushoto), jijini Dar es Salaam leo. Wa tatu ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na wa nne ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya waalikwa, wafanyakazi wa Manispaa za jijini la Dar es Salaam na wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya kumwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi jijini Dar es Salaam leo. 
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa katika hafla ya kumwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi jijini Dar es Salaam leo. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akizungumza wakati wa kumwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kulia), jijini Dar es Salaam leo. 
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kulia), akiwa na Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando.
Wakuu wa Wilaya za Ilala, Raymond Mushi (kushoto) na wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema, wakiwa katika hafla hiyo ya kumwapisha Mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Salum Hapi.
Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando, akielezea kuhusu utaratibu wa kumwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (katikati), wakati wa hafla hiyo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kushoto), akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi katika hafla hiyo. 
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), akijiandaa kuapa. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akiwa tayari kumwapisha.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akimwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), jijini Dar es Salaam leo. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akisaini hati ya kiapo wakati alipomwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando.
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), akisaini hati ya kiapo chake, mara baada ya kuapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia), jijini Dar es Salaam leo. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia), akionesha Katiba ya Jamhuri ya Muungano (kushoto) na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambavyo alikuwa tayari kumkabidhi Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), mara baada ya kumwapisha leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia), akimkabidhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), mara baada ya kumwapisha Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), leo jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), akiabidhiwa maua na Katibu Tawala Msaidizi (Utawala) wa Mkoa wa Dar es Salaam, Elly Mcha. Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando.  
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), akiabidhiwa maua na Katibu Tawala Msaidizi (Utawala) wa Mkoa wa Dar es Salaam, Elly Mcha. 
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akisoma salamu za Mkoa kwa Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akimkabidhi kadi yenye salamu za Mkoa Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi. 
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi, akizungumza mara baada ya kuapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. 
Baadhi ya wageni waliokuwepo katika hafla hiyo, wakisikiliza hotuba ya mkuu huyo wa wilaya. 
Baadhi ya wageni waliokuwepo katika hafla hiyo, wakisikiliza hotuba ya mkuu huyo wa wilaya.  
Baadhi ya wageni waliokuwepo katika hafla hiyo, wakisikiliza hotuba ya mkuu huyo wa wilaya.
Ofisa Habari wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Adrofina Ndandakizye, akichukua habari wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya mpya wa Kinondoni, Ally Salum Hapi (kushoto), akipongezwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad