Matukio : Raila Odinga amtembelea Rais dK. Magufuli nyumbani kwake chato, Mkoani Geita - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


3 Apr 2016

Matukio : Raila Odinga amtembelea Rais dK. Magufuli nyumbani kwake chato, Mkoani Geita

Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiwasili kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Chato Mkoani Geita kwa ajili ya kwenda kumsalimia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Picha na IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga nyumbani kwake Chato mkoani Geita mara baada ya Kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikumbatiana na Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga nyumbani kwake Chato mkoani Geita mara baada ya Kuwasili. Kushoto ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akifurahia.
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli mara baada ya kuwasili Chato.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mke wa Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Bi. Ida Odinga mara baada ya kuwasili Chato Mkoani Geita.
Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiwa na Rais John Magufuli, Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Raila Odinga Bi. Ida Odinga wakisali kwenye makaburi ya familia ya Mhe. Rais Chato Mkoani Geita.
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na mama mzazi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bi Suzana Joseph Magufuli mara baada ya kuwasili Chato Mkoani Geita. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad