Mwanamuziki Ndanda Kosovo amefariki leo asubuhi Jumamosi April 9, 2016
katika hospitali ya taifa Muhimbili. Habari za kifo chake zimethibitishwa
na King Dodoo ambaye ni mmoja ya viongozi wa wanamuziki kutoka Congo.
Katika taarifa yake alisema, Ndanda Kosovo juzi alifikishwa katika
hospitali ya Mwananyamala kwa maradhi ya tumbo, Baadae hali yake
iliendelea kuwa mbaya na siku ya Ijumaa alihamishiwa katika hospitali ya
Muhimbili na baadae kukutwa na mauti leo asubuhi.
Ndanda Kosovo ni mwanamuziki toka Congo aliyewahi kutamba miaka ya 2000 na
bendi ya wajelajela Original.
He is a Tanzanian Journalist , Editor and blogger of Wazalendo 25 Blog which operate since 2006 ; covering International and Local News, including Politics, Sports, Athletics, Events, personalities and positive news happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English Audience.
No comments:
Post a Comment