Madini : Maonyesho ya nne (4) ya Madini ya kimataifa Arusha Gem Fair yafunguliwa jijini Arusha - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


20 Apr 2016

Madini : Maonyesho ya nne (4) ya Madini ya kimataifa Arusha Gem Fair yafunguliwa jijini Arusha


Mkuu wa wilaya ya Arusha,Fadhili Nkurlu akifungua maonesho ya kimataifa ya madini ya Arusha Gem Fair kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Felix Ntibenda leo katika hoteli ya Mount Meru .

Kaimu Kamishna wa Madini nchini,Mhandisi Ally Samaje akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo,alisistiza nia ya serikali kupambana na utoroshwaji wa madini nje ya nchi.

Mwenyekiti wa kamati ya Arusha Gem Fair,Peter Pereira akitoa neno la utanguliza wakati wa ufunguzi wa maonesho ya madini yanayohudhuriwa na waoneshaji na wanunuzi zaidi ya 400 kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Nishati na Madini wakiwa kwenye maonesho ya madini jijini Arusha.

Wadau wa sekta ya madini wakimsikiliza Mkuu wa wilaya.

Wadau wa sekta ya madini wakimsikiliza Mkuu wa wilaya.


Wanunuzi wa madini wakiangalia aina mbalimbali za madini kabla ya kununua.

Madini aina ya Tanzanite 

Madini ya aina mbalimbali ambayo ni kati ya yanayooneshwa kwaajili ya kutafutiwa soko.

Mkurugenzi wa kampuni ya Ruvu Gemstone Mining Company Limited,Dimitris Mantheakis(kushoto)akiwa na wateja wanaongalia aina za madini.

Imeandaliwa na www.rweyemamuinfo.blogspot.com,Arusha

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad