Matukio : Ujumbe kutoka kwa Bi. Irina Bokova ,katika siku ya ushauri duniani, 21 machi 2016 - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


21 Mar 2016

Matukio : Ujumbe kutoka kwa Bi. Irina Bokova ,katika siku ya ushauri duniani, 21 machi 2016

Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Bi. Irina Bokova.
Shakespeare, mwandishi maarufu kutoka Uingereza aliyefariki yapata miaka 400 iliyopita, aliandika katika tamthilia yake inayojulikana kama “A Midsummer Night's Dream” kuwa, “Jicho la mshairi, hutazama kwa umakini na undani, kutoka mbinguni hadi duniani, na duniani hadi mbinguni. Na kama vitu vya kufikirika vusivyofahika vinavyoumbika katika mawazo, ndivyo kalamu ya mshairi inavyogeuza mawazo hayo kuwa katika maumbo yasiyoweza kudhaniwa”
Kwa kuwatambua na kuwaheshimu wanaume na wanawake, ambao chombo chao pekee ni uhuru wa kujieleza, watu wanaofikiria na kuchukua hatua, UNESCO inatambua thamani ya ushairi kama ishara ya ubunifu wa mwanadamu. Kwa kutoa umbo na maneno kwa mambo ambayo katika hali ya kawaida hayakuwa nayo, kama vile uzuri usiopimika unaotuzunguka na mateso na taabu kubwa za dunia, mashairi yanachangia upanuzi wa ubinadamu wetu, kwa kusaidia kuongeza nguvu za ubinadamu wetu, mshikamano na kujitambua.
Sauti zinazobeba ushairi husaidia kukuza upana na utofauti wa lugha na uhuru wa kujieleza. Sauti hizi hushiriki katika jitihada za kimataifa kuelekea elimu ya kisanii na usambazaji wa utamaduni. Wakati mwingine, neno la kwanza la shairi latosha kabisa kurejesha kujiamini pale mtu anapokuwa anakabiliwa na upinzani na kupelekea kuiona tena njia ya matumaini pale unapopambana na unyama. Katika zama hizi za teknolojia na uharaka wa maisha ya kisasa, ushairi hufunya nafasi kwa ajili ya uhuru na kuvinjari, hali iliyo ndani ya utu wa mwanadamu. Kutoka Arirang za huko Korea hadi Pirekua za Mexico, nyimbo za Hudhud za jamii ya watu wa Ifugao, Alardah za Saudi Arabia, Koroghlu za jamii ya watu wa Turkmenistan na maeneo ya Iran na Afghanistan, na Aitysh za watu wa Kyrgyz, kila utamaduni una aina ya sanaa yake ya ushairi inaoutumia kupeleka na kusambaza maarifa, maadili ya kijamii na kiutamaduni na kumbukumbu za pamoja, ambayo huimarisha kuheshimiana, mshikamano wa kijamii na kutafuta amani.
Leo hii, nawapongeza washairi, wasanii, waghani, na wale wote ambao sauti zao, bila ya wao wenyewe kujulikana, wamejitoa, kwa na kupitia ushairi, kutoa masomo katika hali ya taswira au ya uwazi, katika bustani au katika mitaa. Ninatoa wito kwa nchi wanachama wote wa UNESCO kuunga mkono juhudi hizi za ushairi, ambao una uwezo wa kutukusanya pamoja, bila kujali asili au imani, kwa lile lililo hasa katika kiini cha ubinadamu

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad