Matukio : Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa apokea misaada mbalimbali kwa waathirika wa Mvua wilayani ruangwa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


28 Feb 2016

Matukio : Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa apokea misaada mbalimbali kwa waathirika wa Mvua wilayani ruangwa



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa ambao unafanywa kwa ufadhili wa kampuni ya HUAWEI ya China , kijijini hapo, Februari 28, 2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Jordan Lugimbana.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea hundi ya shilingi milioni tisa kutoka kwa Mtalaam wa Ufundi wa Kampuni ya simu ya Halotel wa mkoa wa Lindi, Tran The Hoang ili ziweze kugharimia malipo ya kadi za bima ya Afya kwa baadhi ya wakazi wa kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa. Alikuwa katika ziara ya siku moja wilayani humo Februari 29, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa ma Mwanaidi Mussa na Mkussa Lukoloma (kushoto) wote wa kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwabaada ya kuwakabidhi kadi zao za bima ya Afya ambazo zimegharimiwa na Kampuni ya Simu ya Halotel iliyochangia shilingi milioni tisa kuwawezesha wakazi wa kijiji hicho kufaidi huduma za Bima ya Afya, Februari 28, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea msaada wa vyakula na nguo kutoka kwa Mwenyekiti watu waliojitotelea kusaidia waliopatwa na maafa ya mvua katika kijiji cha Mtondo wilayani Ruangwa wakati Waziri Mkuu alipokwenda kijijini hapo kuwapa pole wananchi Februari 28, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wananchi wa Ruangwa baada ya kuwasili mjini hapo kwa ziara ya siku moja Februari 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad