Bi. Sangita Reddy, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali za Apollo
Na Mwandishi Wetu ,
Kurahisisha huduma za afya ulimwengu kote, watojia wakubwa wa huduma za afya kundi la hospitali za Apollo limebuni njia mpya madhubuti ya utoaji wa huduma za afya inayoitwa; Ask Apollo, njia bora mpya mahususi kwa wagonjwa walio mbali. Hii inathibitisha kupiga hatua zaidi kwa hospitali za Apollo na katika uwanja wa afya ulimwenguni.
Jitihada
hizi kutoka hospitali za Apollo zitajenga mahusiano rahisi ya
mgonjwa-huduma zitakazo mpa mgonjwa mbadala wa kuwasiliana na daktari
mahali popote na muda wowote watakao kubaliana. Kupitia Ask Apollo, mgonjwa
anaweza kuweka miadi na daktari wa mambo ya familia,mlo kamili na mambo
ya afya, ushauri kutoka kwa wataalam au bodi ya wataalam kutokana na
uhalisia wa tatizo.
Akitoa maoni katika ufunguzi, Ms. Sangita Reddy, mkurugenzi mtendaji wa hospitali za Apollo alisema “kupitia Ask Apollo, tunaendeleza kundi la Apollo litakaloacha urithi mkubwa kwenye kutengeneza mandhari na kuchangia kuinua viwango vya utoaji huduma za afya. Hospitali za Apollo zina nia ya kuleta mapinduzi kupitia teknolojia kupitia program ya Ask Apollob ambapo mgonjwa anaweza hadi kuchagua daktari anayempenda na kupanga muda atakao hitaji kuonana nae. Ask Apollo ni 100% huduma ya kimtandao hivyo inaondoa uhangaikaji wa kusafir kwenda kliniki au hospitali na kukaa kwenye foleni ndefu.”
Kujifunza mengi kuhusu “Ask Apollo”, mtumiaji anaweza kuingia kwa www.askapollo.com na kupata huduma za Ask Apollo, aliongeza Mkg. Sangita Reddy.
Watanzania wanashauriwa kufaidika na huduma za kiafya kutoka Ask Apollo pindi wanahitaji huduma bora za kiafya kwa magonjwa makubwa au sugu. Ask Apollo
ni huduma yenye gharama nafuu lakini pia inawafaidisha wagonjwa waliopo
mbali. Wagonjwa kutoka Tanzania wanaweza kupata huduma hii kutoka kwa
wataalam muda wote masaa 24 kwa wiki kutokana na ukubwa wa tatizo.
Huduma hii ya kimtandao inaokoa muda, pesa, na usumbufu wa watanzania
kusafiri mara kwa mara kwa ajili ya huduma za afya hospitali za Apollo.
Hospitali za Apollo zimechukua
hatua madhubuti kwenye kuboresha huduma za afya. Umakini katika zoezi
hili umeongeza kasi kwenye kupata taarifa na muda wa kuzipata katu ya
mgonjwa na daktari. Nia hii ya hospitali za Apollo ni hatua katika kuboresha upatikanaji bora wa huduma za afya ulimwenguni.
Huduma ya Ask Apollo inalenga
mambo makuu yafuatayo; mfumo wa upumuaji na moyo (Cardiology), afya ya
uzazi wa mama (Gynecology), mfumo wa fahamu na ubongo (Neuro Surgery),
mfumo wa mkojo (Urology), daktari wa watoto (Pediatrician),maumivu ya
miguu na viungo (Rheumatology), matatizo ya ngozi (Dermatology),
matatizo ya akili (Psychiatry), matatizo ya nevu (Nephrology), upasuaji
wa uvimbe (Surgical Oncology), miale kwa ajili ya kuondoa uvimbe
(Radiation Oncology), matibabu ya uvimbe (Medical Oncology), madawa ya
ndani na upasuaji wa uvimbe katika kichwa na shingo.
Kupitia
uwanja huu wa huduma za kiafya, mtu anaweza kuchagua daktari anayemtaka
au mtaalam kutokana na aina ya ugonjwa ulio nao, unaweka taarifa zako
na kuonana na daktari, program hii itasaidia mgonjwa kupata aina gani za
dawa atumie.
Kwa
miongo iliyopita, ulimwengu wa afya umekumbana na mabadiliko makubwa ya
maendeleo ya kiteknolojia na pia ubunifu uliopelekea mapinduzi katika
kumpata daktari na matibabu kwa wagonjwa. Mapinduzi haya kwenye maeneo
tofauti ya afya yamesaidia kuimarisha huduma za afya na kuleta matokeo
mazuri kwa wagonjwa.
Ongezeko
kubwa la utoaji huduma bora za afya na upanukaji wa matumizi yake
umechangia sio tu kwenye kuwakutanisha madaktari katika fani zao bali
pia kutengeneza uwanja mzuri wa daktari kukutanishwa na wagonjwa.
Kuhusu Hospitali za Apollo
Hospitali ya Apollo ilifunguliwa mnamo mwaka 1983, na kutoka kipindi hicho imekuwa ikiendeshwa kwa kauli mbiu isemayo "Dhamira
yetu ni kuleta huduma ya kisasa karibu kabisa na walengwa. Tunajitolea
kutoa huduma bora na mafanikio katika elimu na utafiti kwa ajili ya
jamii ya kibinadamu".Katika miaka 30 tokea
kuanzishwa kwake, hospitali ya Apollo imeandika historia kubwa kupata
kuonekana nchini India. Ni moja ya kampuni kubwa ya Afya katika bara la
Asia, na pia imeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya nchini
india.
Katika
safari yake, imeweza kuboresha maisha ya watu wapatao milioni 39 kutoka
nchi 120.Inatoa huduma maalum 52 na vitanda vya upasuaji 710.Imefanya
upasuaji wa moyo wenye kufikia idadi ya watu 152,000 na panuzi 125, 000
za mishipa myembamba.Imefanya upasuaji wa wa viungo unaopita kiasi cha
idadi ya watu 10,000, upasuaji wa uvimbe wa ubongo, uti wa mgongo na
zaidi.Taasisi ya Apollo ni moja ya taasisi zinazoongoza nchini india,
zikiwa na teknolojia za kisasa kama Novalis TX, PET MRI na Upasuaji
unaotumia mashine za kiroboti.
No comments:
Post a Comment