Habari zilizotufikia na kuthibitishwa na Katibu wa
Mbunge wa Arumeru Mashariki zinaeleza kuwa Mbunge Joshua Nassari pamoja
na abiria wengine wawili na rubani wao wamenusurika kifo baada ya
helkopta waliyokuwa wakisafiria kuhamasisha uandikishaji Jimboni
kuanguka jioni ya 7/7 /2015.
Taarifa zinaeleza kuwa helkopta hiyo imeanguka katika kijiji cha Leguruki Wilayani Arumeru Mashariki baada ya hali ya hewa kuwa mbaya.
Nassari na majeruhi wengine wamewahishwa hospitali ya Selian Jijini Arusha kwa matibabu ya majeraha kiasi waliyoyapata.
Blog hii inaendelea kufuatilia tukio hili kwa karibu na kukujuza kila kitu.
Taarifa zinaeleza kuwa helkopta hiyo imeanguka katika kijiji cha Leguruki Wilayani Arumeru Mashariki baada ya hali ya hewa kuwa mbaya.
Nassari na majeruhi wengine wamewahishwa hospitali ya Selian Jijini Arusha kwa matibabu ya majeraha kiasi waliyoyapata.
Blog hii inaendelea kufuatilia tukio hili kwa karibu na kukujuza kila kitu.




No comments:
Post a Comment