Vifaa vya Michezo :Waziri Dk. Fenella Mukangara apokea msaada wa vifaa vya michezo kutoka kwa Serikali ya China - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


18 Jan 2015

Vifaa vya Michezo :Waziri Dk. Fenella Mukangara apokea msaada wa vifaa vya michezo kutoka kwa Serikali ya China


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kukabibidhiwa msaada wa vifaa vya michezo kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China  jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Balozi wa China hapo nchini Lu Youqing na Mwakilishi Mkuu wa Wafanyabiashara kutoka China waishio nchini Lin Zhiyong. Jumla ya vifaa kumi na nne vimetolewa ambavyo ni Roboti ya kujifunzia mpira wa Meza, Kifaa cha kupimia upepo kwa ajili ya Riadha,Nyavu ya mpira wa Meza, Mashine ya kupimia Uzito,Ulingo wa Ngumi,Kompyuta,Printa, Radio Call, mashine ya kutafsirina kuhesabu matokeo katika riadha na nyaya za umeme vyenye thamani zaidi ya 200.
Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kukabibidhi msaada wa vifaa vya michezo kwa Serikali ya Tanzania vilivyopokelewa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (hayupo pichani)  jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) akicheza Mpira wa Meza na Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing (kulia) wakati wa hafla ya kukabibidhiwa msaada wa vifaa vya michezo kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China jijini Dar es Salaam.
Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing akielezea namna mmtambo wa Radio Call unavyofanya kazi, katika mwenye blauzi ya kitenge Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara, na Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo Bibi. Juliana Yassoda.
Ulingo wa kisasa uliokabidhiwa kwa Serikali ya Tanzania kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China leo jini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) akibadilishana hati ya makabidhiano ya vifaa vya michezo na Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing (kulia) wakati wa hafla ya kukabibidhiana vifaa hivyo leo jijini Dar es Salaam. Picha na Frank Shija.

Na Benjamin Sawe, WHVUM

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imepokea msaada wa vifaa mbalimbali vya mchezo wa ngumi na riadha kutoka kwa Serikali ya Watu wa China vyenye jumla ya thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200.

Akizungumza katika makabidhiano hayo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr. Fennela Mukangara alisema msaada huo ni sehemu ya kuboresha tasnia ya michezo ikiwa ni pamoja na kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu baina ya nchi hizo mbili.

“Msaada huu ni kiashirio tosha kwa wananchi wa nchi zote mbili na umekuwepo ukiendelea kuimarika na tunazo fursa za kuendeleza ushirikiano huu kwa manufaa ya wananchi wetu”.Alisema Mheshimiwa Mukangara.

Aidha alimuhakikishia Mheshimiwa Balozi wa China kuwa Watanzania wanathamini mchango mkubwa wenye lengo la kuendeleza michezo hapa nchini kwani China na Tanzania zina historia ya pamoja ya takribani ya miaka 50 mpaka sasa.

Alisema kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imewasilisha kwenye ofisi ya Ubalozi wa China mapendekezo ya kuendeleza ushirikiano kupitia sekta ya michezo ambapo matumaini yake ni kuwa kwa kupitia maeneo hayo zitapatikana fursa zaidi kwa vijana kuendeleza ushirikiano baina ya nchi mbili kupitia michezo ikiwa ni pamoja na kujifinza mambo muhimu katika tasnia ya Michezo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mh. Lu Youqing alisema Serikali yake itaendelea kuwa na ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwa ni ishara ya kudumisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na “Table Tennis 2”, Wind Speed Gage Device 2, “UPS 1, Table Tennis Net” 7, “Electronic Weigher 2”, Computer 1, “Table Tennis Balls”, “Boxing Ring 2”, “Table Tennis 5”, “Printer 1”, “Electronic Cable 6”, “Radio Call 2”, “Anemograph 2”, na Electric Timing and Scoring Interpretation Device For Finishing line 1” ambapo jumla yake ni zaidi ya shilingi milioni 200.

Mpaka sasa Serikali ya China imeshaipatia msaada Serikali ya Tanzania jumla ya shilingi bilioni moja ili kuendeleza sekta mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad