Meneja
wa ATM na Kadi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Wambura John
(kushoto) akiweka pesa kwa kutumia ATM katika hafla ya uzinduzi wa
huduma ya kuweka pesa (deposit) kwa kutumia mashine za ATM ya benki ya
NBC jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati ni mteja wa benki
hiyo, Francis Xavier na kulia ni Meneja Huduma za Jamii wa NBC, Irene
Peter
Mteja
wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Francis Xavier (kushoto) akiweka
pesa (deposit) katika mashine ya ATM ya benki hiyo wakati wa uzinduzi
rasmi wa huduma hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati ni
Meneja wa ATM na Kadi wa NBC, Wambura John (katikati) na Meneja Huduma
za Jamii wa benki hiyo, Irene Peter.
BENKI
ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma mpya ya kuweka fedha kwenye
mashine za ATM jijini Dar es Salaam katika juhudi za benki hiyo
kuboresha huduma za kifedha nchini.
Kuanzishwa
kwa huduma hiyo kunathibitisha malengo ya benki hiyo ya kutoa huduma
sahihi na ya wakati kwa wateja wake nchini nzima na huduma hii ya kuweka
fedha kwenye mashine za ATM itakuwa ikipatikana masaa 24 kila siku.
“Uanzishwaji
wa huduma hii ya kuweka fedha kwenye mashine za ATM itawahakikishia
wateja wetu kupata huduma sahihi na ya uhakika wakati wowote, uwekaji wa
fedha katika mashine hizi ni wa haraka, rahisi, na inaokoa muda wa
kupanga foleni ndani ya benki,” alisema Mkuu wa Njia Mbadala za Kibenki
wa NBC, Raymond Mutagahywa.
Aliongeza
kwamba huduma hii ya NBC kwa mtumiaji yeyote ni ya kirafiki na rahisi
sana ni kwamba mtu anahitajika kufanya mambo machache tu baada ya
kuingiza kadi yake ya ATM na kuchagua sehemu ya kuweka fedha na mashine
ya ATM itafunguka ili mteja aweze kuweka fedha zake.
Benki
hii ya NBC imeanza huduma hiyo kwenye matawi yake ya jijini Dar es
Salaam, karikaoo, kinondoni, Mlimani City na Tawi la Makao makuu ambayo
mteja anaweza kuweka mpaka shilingi za kitanzania 1.5milioni kwenye
mashine za ATM.
Uzinduzi
huu wa kuweka fedha kwenye mashine za ATM ulifanyika katika Tawi la
benki hiyo la Mlimani city na kushuhudiwa na wateja kadhaa wa benki hiyo
na walivutiwa na jisni mashine zinavyotumika kuweka fedha moja kwa
moja.
“Hizi
mashine za ATM zimekuja wakati muafaka kabisa hasa kwa wateja wetu ambao
wanaendelea na biashara zao wakati ambao matawi mengi yamekuwa
yamefungwa lakini huduma hii itawawezesha kufanya shughuli zao za
kibenki za kuweka fedha bila matatizo,’ aliongeza Neema Munisi Mhasibu
wa Tawi la Mlimani City.
“Tumeanzisha
na kuzindua huduma hii ya kuweka fedha kwenye mashine za ATM kwenye
matawi manne tu jijini Dar es Salaam na tutaendelea kufungua na
kusambaza huduma hii ya kuweka fedha kwenye mashine hizi nchini nzima,”
aliongeza Munisi
Kwa
wake Mteja wa benki hiyo aliyejaribu huduma hiyo mpya, Franscis Xavier
Momanyi alisema kwamba kwa huduma hiyo mpya kutoka benki hiyo
itawahikishia wateja wote uhakika wa kupata fedha au kuweka fedha wakati
wowote pindi watakapohitaji.
Alisema
kwamba ni muhimu kwa benki hiyo kupeleka kwa haraka huduma hiyo ya
kipekee kwenye matawi mengine nje ya mkoa wa Dar es Salaam ili wateja
wengine wapate fursa ya kutumia huduma hiyo.
No comments:
Post a Comment