KAMA UNA KIPAJI CHA KUIGIZA, KAMATA FURSA : PROIN PROMOTIONS LIMITED INASAKA VIPAJI VYA KUIGIZA NCHINI, - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Friday, 7 March 2014

demo-image

KAMA UNA KIPAJI CHA KUIGIZA, KAMATA FURSA : PROIN PROMOTIONS LIMITED INASAKA VIPAJI VYA KUIGIZA NCHINI,

IMG_7804

Meneja wa Mradi wa Kusaka Vipaji Vya Uigizaji Tanzania (Tanzania Movie Talents) Bw Joshua Moshi akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wakutambulisha kampeni mpya ya kusaka Vipaji vya uigizaji kutoka kampuni ya Proin Promotions Limited mapema leo katika Ofisi za Proin Promotions Limited, Mikocheni, Mtaa wa Ursino, Pembeni ni Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited Bw Evance Stephen. .com/blogger_img_proxy/
Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited, Bw Evance Stephen (katikati) akielezea jinsi ya Kampuni ya Proin Promotions itakapozunguka katika Mikoa ya Tanzania Kwaajili ya Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania kwenye Mkutano na waandishi wa Habari mapema leo katika Ofisi za Proin Promotions Limited, Mikocheni, Mtaa wa Ursino,, Shindano litaendeshwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited.
IMG_7843
Meneja Mradi wa Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania (Tanzania Movie Talents) Bw Joshua Moshi (wa kwanza Kushoto) pamoja na Meneja Masoko wa Proin Promotions Limited, Bw Evance Stephen wakisikiliza Maswali kutoka kwa waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo katika Ofisi za Proin  zilizopo Mtaa wa Ursino Mikocheni.
IMG_7849
Muigizaji wa Filamu za Kitanzania Single Mtambalike almaarufu Rich Rich ambae pia ni mmoja wa majaji katika Shindano la kusaka vipaji vya uigizaji lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents lililopo chini ya Kampuni ya Proin Promotions Limited akiongelea jinsi washindi watakavyopatikana katika shindano hilo linalotarajia kuanza tarehe 1 Aprili 2014.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *