ALPHONCE FELIX WA ARUSHA AVUNJA REKODI KATIKA MBIO ZA ROCK CITY MARATHON 2013 - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

28 Oct 2013

ALPHONCE FELIX WA ARUSHA AVUNJA REKODI KATIKA MBIO ZA ROCK CITY MARATHON 2013


Mshindi  wa kwanza wa mbio za Rock City Marathon 2013 kilomita 21 kwa upande wa wanaume Alphonse Felix kutoka mkoani Arusha akimalizia mbio hizo kwenye uwanja wa CCM Kirumba ambapo alitumia saa 1:02:17 na kufanikiwa kuvunja rekodi iliyowekwa mwaka jana na Opio Chacha aliyetumia saa 1:05:47.
Afisa Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa hifadhi wa jamii NSSF  Bi. Theopista Mheta akimkabidhi zawadi ya shilingi 1,500,000/= mshindi wa kwanza mbio za Rock City Marathon kilomita 21kwa upande wa wanaume Alphonse Felix ambaye pia alijinyakulia zawadi ya tiketi ya ndege toka moja wa wadhamini wa mbio hizo Precission Air, ya kuelekea Dar es Salaam na kurudi mkoani kwake Arusha.
Afisa Mauzo wa King’amuzi cha Continental, Dominic Kiluma akikabidhi zawadi ya king’amuzi kwa Joel Kimbiaye toka Kenya mara baada ya kuibuka mshindi wa nafasi ya pili mbio za Rock City Marathon 2013 ambapo pia mshiriki huyo alijinyakulia kitita cha shilingi 900,000/=.
Afisa Mahusiano na Masoko wa Mfuko wa hifadhi wa jamii NSSF Bi. Theopista Mheta  akikabidhi zawadi ya shilingi 700,000/= mshindi wa tatu katika mbio za Rock City Marathon  kilomita 21, Andrew Sambu ambaye pia alijinyakulia king’amuzi cha Continental.
Afisa Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa hifadhi wa jamii NSSF  Bi. Theopista Mheta akimkabidhi zawadi ya shilingi 1,500,000/= mshindi wa kwanza mbio za Rock City Marathon kilomita 21 kwa upande wa wanawake Vicoty Chepkemoi kutoka Kenya.
Afisa Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa hifadhi wa jamii NSSF  Bi. Theopista Mheta akimkabidhi zawadi ya shilingi 900,000/= mshindi wa pili wa mbio za Rock City Marathon kilomita 21 wanawake Sarah Ramadhan ambaye pia alinyakuwa king’amuzi cha Continental.
Afisa Mauzo wa King’amuzi cha Continental  Dominic Kiluma akikabidhi zawadi ya king’amuzi kwa mshindi wa tatu mbio za Rock City Marathon 2013 wanawake, Zakia Mrisho ambaye pia alijinyakulia kiasi cha shilingi 700,000/=
Washiriki wa Rock City Marathon 2013 wakichuana vikali kuisaka nafasi za ushindi wa mbio hizo ili kujinyakulia zawadi mbalimbali zilizoanishwa na wadhamini wa michuano hiyo ambao iliandaliwa na ampuni ya Capital Plus International Limited kwa kushirikaina na wadhamini mbalimbali.
Washiriki kutoka Australia wakimaliza mbio za kilomita 21.
Baadhi ya raia wa nchi za kigeni wakipumzika baada ya kumaliza mbio za Rock City Marathon
Meneja Uhusiano wa Airtel  Bw, Jackson Mmbando akimpongeza mshindi wa kwanza wa mbio za kilomita 2,  Benedicto Mashauri wa mwanza, baada ya kuwashinda watoto wenzake 284 walioshiriki mbio za Rock City Marathon 2013
Mkurugenzi wa Club ya Holili Youth Athletics iliyoko mkoani Kilimanjaro wilayani Rombo Domian Rwezaura Janand, akitamba mara baada ya mashindano kwa washiriki toka kambi yake kufanya vyema kwenye mbio za Rock City Marathon 2013
Sehemu ya watoto waliowakilisha walioshiriki mbio za Rock City Marathon 2013.

Mbio za Rock City Marathon 2013 zafana
WANARIADHA Alphonce Felix kutoka Arusha na Vicoty Chepkemoi kutoka Kenya wameibuka vinara katika mashindano ya riadha ya kilometa 21 yanayojulikana kama ‘Rock City Marathon 2013’ yaliyofanyika Jijini Mwanza jana Jumapili nakujinyakulia Shilingi milioni moja na nusu (Sh 1.5 m) kila mmoja.
Alphonce alishinda mbio hizo kwa upande wa wanaume baada ya kutumia saa 1:02:17 hivyo kuvunja rekodi iliyowekwa mwaka jana na mwanariadha Kopiro Chacha aliyetumia 1:05:00, huku Chepkemoi aki kutumia 1:12:44.
Nafasi ya pili alishika Joel Kimtiae wa Kenya kwa upande wa wanaume na Sarah Ramdhani kutoka Arusha kwa upande wa wanawake, wakifuatiwa na Sambo Andrea kwa upande wa wanaume na Zakia Mrisho kwa upande wa wanawake wote wakitokea Tanzania.
Zaidi ya wanariadha 1090 walijitokeza kushiriki mashindano hayo yanayoandaliwa na kampuni ya Capital Plus International kwa mwaka wa tano mfululizo.
Wambura Lameck kutoka Holili alingara katika mbio za kilometa tano huku Dotto Ikangaa kutoka Arusha akishika nafasi ya pili .
Kwa mujibu wa waratibu wa mbio hizi, udhamini waliopata kutoka kwa wadamini ambao ni, Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF), Africa Barrick Gold (ABG), Precision Air, Airtel kupitia Airtel Money, TANAPA, Bank M, PPF, Nyanza Bottling Ltd, New Mwanza Hotel, Sahara Communications, Continental Decoders na Umoja Switch, umewawezesha kuboresha tuzo kwa washiriki pamoja na kufanya maadalizi mazuri yanayozingatia sheria za riadha.
Washiriki na washabiki wa mbio za Rock City za mwaka huu walipata kuburudishwa na kikundi cha Sanaa cha Bujora ambacho kilionyesha umahiri wake wa kuonyesha utamaduni wa kitanzania kupitia dansi.          
Mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Mwanza Bw Kizito Bahati (Afisa michezo Manispaa ya Ilemela), mbali na kutaka washiriki kutoka kanda ya ziwa kuchangamkia fursa inayoletwa na mbio hizo, pia aliwataka viongozi wa vyama vya riadha kuwa na program endelevu ya kukuza mchezo wa riadha kwa kushirikiana na Maafisa Michezo wa Mikoa na Wilaya ili waweze kupata fursa ya kufikisha na kuufundisha mchezo huu katika shule ambako ndio chimbuko la vipaji vya michezo.
“Nawashukuru sana waandaaji wa mbio hizi za Rock City Marathon kwa kuweza kuandaa shindano ambalo limeweza kutusaidia sisi wadau wa riadha kugundua vipaji vingi ambavyo tunavyo hapa nchini. Hivi vipaji vinastahili kukuzwa. Hivyo basi natoa wito kwa watu wote wenye dhamana ya michezo kutumia mbio hizi kama chambo cha kuweza kutambua vipaji vingi vya riadha ambavyo vinahitaji kuendelezwa kwa manufaa ya taifa,” alisema Bw Kizito.
Pamoja na hayo mashindano haya yameweza kufanikiwa kwa udhamini wa makampuni mbalimbali nayapongeza kwa juhudi zao za kuweza kuinua michezo hapa mkoani Mwanza na Tanzania kwa ujumla. Nayaomba na makampuni mengine kujitokeza kudhamini michezo hii kwani fursa kwao katika kutangaza bidhaa zao.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Suleiman Nyambui alisema Rock City Marathon imeonyesha kukua kila mwaka, kwa kuwa inauwezo wa kukimbiza mbio za ngazi zote; nusu marathon, kilometa tano, kilometa tatu kwa walemavu, kilometa tatu kwa wazee na kilometa mbili kwa watoto.
Alisema Shirikisho limezingatia usimamizi mzuri wa Rock City Marathon na lipo tayari kutoa kibali kitachacho iwezesha kampuni ya Capital Plus International kuandaa mbio ndefu za kilometa 42 (full Marathon) watu wakiweza kuhamasika na kushiriki kwa wingi.
Washiriki kutoka mikoa mbali mbali waliweza kushiriki na wageni kutoka nchi kama Kenya and Uganda, India, Canada, Australia, Africa Kusini, Rwanda, pia walishiriki.
Mbali na medali walizopata washindi hawa, zawadi za fedha taslimu zilitolewa ambapo washindi wa pili katika mbio za kilometa 21, upande wa wanaume na wanawake walipata 900,000/-  na vingamuzi vya Continental kila mmoja. 
Washindi wa tatu kilometa 21 wakiondoka na kingamuzi na 700,000/-  na decoda za Continental kila mmoja kwa upande wa wanaume na wanawake.
Muhindiro Yusto kutoka Mwanza aliyeshinda kilometa tatu kwa upande wa wazee na Benard Samike wa Mwanza kwa upande wa watu wenye ulemavu .
Kwa upande wa watoto ambao walikimbia kilometa mbili, Benedicto Mashauri wa mwanza alishika nafasi ya kwanza huku Suzana Madary wa Mwanza akingara kwa upande wa wasichana. Picha zote na G sengo Blog

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633