BWANA HARUSI ANUSURIKA KIFO SIKU MOJA KABLA YA NDOA YAKE -MBEYA - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Tuesday, 18 December 2012

demo-image

BWANA HARUSI ANUSURIKA KIFO SIKU MOJA KABLA YA NDOA YAKE -MBEYA


DSC00062
Bwana harusi Emmanuel Mwangosi akiwa na mkewe Magreth  Mtebe mara tu baada ya kufunga pingu za maisha jana katika kanisa la Agape jakaranda jijini mbeya. Bwana harusi anaonekana na majeraha baada ya kunusurika kifo katika ajali ya pikipiki na gari usiku wa kuamkia Jumapili ambayo alifunga ndoa.
DSC00099
Hii ndiyo ajali aliyopata bwana harusi emmanueli aligongwa na gari aina ya Toyota GX 100  Emmanuel yeye alikuwa anaendesha pikipiki usiku wa kuamkia jumamosi mida ya saa sita nanusu usiku alikuwa anaenda kwenye mkesha kanisani ndiyo ajali hiyo ikatokea maeneo ya mafiati mbeya wengi wa mashuhuda hao walijua mwendesha pikipiki hiyo amekufa papo hapo 
DSC00105
Hii ndiyo hali halisi iliyotokea siku hiyo ya ajali mbeya yetu tulifika usiku huo eneo la tukio na kukuta tayari majeruhi wametolewa na kupelekwa katika hospitali ya rufaa Mbeya ndipo jana tukaamua kufuatilia majeruhi hao na kukuta kuwa Emmanueli ameruhusiwa kwa muda akafunge ndoa kwani jana ilikuwa siku ya yeye kuoa ndipo tukaenda kufuatilia harusi hiyo  katika kanisa la agape 
DSC00092
DSC00006
Bwana harusi Emmanueli na mpambe wake Frank wakiingia kanisani
DSC00010
Hakika ni furaha hapa bwana harusi anamtambua mkewe kwa kumfunua shela kabla ya ndoa kufungwa
DSC00055
Sasa bana na bibi harusi wanaingia kanisani tayari kwa ibada ya ndoa
DSC00016
Mchungaji Emmanuel Mwasota toka E.A.G.T toka DSM ndiyo aliyofungisha ndoa hiyo
DSC00023
Hapa bwana harusi akimvisha mkewe pete  huku bibi harusi akiwa katika furaha kubwa na kumshukuru mungu kwa kumuepusha mumewe katika ajali iliyotokea
DSC00028
Hapa wakipata mibaraka ya ndoa kutoka kwa wachungaji mbalimbali wa kanisa hilo la AGAPE
DSC00030
Sasa tu mwili mmoja kitakachotutenganisha ni kifo tu jina la bwana libarikiwe
DSC00038
Bwana harusi akipokea cheti cha ndoa toka kwa mchungaji Mwasota
DSC00047

DSC00086
Wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kufunga ndoa
DSC00074
Maharusi wakiwa na familia na wazazi wao
DSC00109
Sherehe fupi ya kuwapongeza maharusi ilifanyika katika bustani ya ccm jijini mbeya
DSC00111
Ndugu jamaa na marafiki walihudhuria sherehe hiyo ingawa maharusi hawakuweza fika kwenye sherehe hiyo kutokana hali yake haikuwa nzuri alihitaji kupumzika na kurejea tena hospitali kuendelea na matibabu
DSC00112
Mungu bado ni mwaminifu sana,waalikwa wa kila kwa furaha kabisa : Picha na Gwasa wa Mbeya yetu

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *