Tanga wapagawa na Tamasha la FIESTA 2012 - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


27 Aug 2012

Tanga wapagawa na Tamasha la FIESTA 2012

Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego pichani kati mwenye kipaza sauti akisoma namba za washindi waliojinyakulia piki piki mbili zilizotolewa na kampuni ya Push Mobile, wa tatu kulia ni Meneja Masoko wa kampuni ya Push Mobile,Rugambo Rodney na mwisho kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Clouds Media Group,Joseph Kusaga,na nyuma kabisa ni Mkurugenzi wa utafiti Clouds Media Group, Ruge Mutahaba pamoja na Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti,Ephrahim Mafuru wakishuhudia tukio hilo usiku huu kwenye uwanja wa Mkwakwani ambako tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linafanyika.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Clouds Media Group, Joseph Kusaga usiku huu mara baada ya kuwataja washindi waliojishindia piki piki mara baada ya kuchezeshwa bahati nasibu,wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea,pichani kati ni Afisa Mahusiano wa Clouds Media Group, Simon Simalenga.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nuru akitumbuiza jukwaani usiku huu na shabiki wake mbele ya wakazi wa jiji la Tanga wanaondelea kutiririka ndani ya uwanja wa Mkwakwani ambako tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
  Rachel wa THT,akifanya vitu vyake kwenye jukwaa la Fiesta Tanga.
Pichani shoto ni Mkurugenzi wa Masoko, Ephrahim Mafuru, Mkuu wa Vipindi Clouds FM,Sebastian Maganga sambamba na Meneja wa bia ya Serengeti,Allan Chonjo wakiwa katika picha ya pamoja ndani ya uwanja wa Mkwakwani wakati tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kurindima.
Dj Zero kutoka Clouds FM akikamua.
Sehemu ya umati wa wakazi wa Tanga wakifuatilia kwa makini makamuzi ya Fiesta 2012

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad