Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa Akuatana na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Monduli Kujadili Hali ya Elimu ya Shule Hiyo - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


22 Mar 2012

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa Akuatana na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Monduli Kujadili Hali ya Elimu ya Shule Hiyo


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza kwa kusisitiza wakati wa mkutano wake na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Wilayani Monduli kuhusiana na hali ya elimu katika shule hiyo kutoridhisha na kupelekea wanafunzi wengi wa shule hiyo kufeli kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.Mkutano huo umefanyika leo shuleni hapo,ambapo walimu wa shule hiyo walitoa changamoto mbali mbali wanazomabiliana nazo.Mh. Lowassa amewaasa walimu wa Shule hiyo kuwa wafanye kazi kwa juhudi ili kuwaandaa vijana wa taifa la baadae.Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo,Bw. Joseph Lukumay.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Shule ya Sekondari ya Engutoto,Bw. Joseph Lukumay akitoa maelezo mafupi na kuwataka walimu wa shule hiyo kuanza kuzungumzia ni kwanini shule yao imefanya vibaya kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.
 Afisa Elimu Wilaya ya Monduli,Bw. Shaaban Mngunye (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (wa pili kulia) wakati wa mkutano na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Wilayani Monduli.Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo,Mwl. Ally Muyago na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo,Bw. Joseph Lukumay.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Shule ya Sekondari ya Engutoto iliyopo Wilayani Monduli Mkoani Arusha,Mwl. Ally Muyago akitia taarifa fupi ya shule yake kwa Mh. Edward Lowassa ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo la Monduli,wakati wa mkutano wake na Walimu wa Shule hiyo kuhusiana na hali ya elimu katika shule hiyo kutoridhisha na kupelekea wanafunzi wengi wa shule hiyo kufeli kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.
 
Afisa Elimu Wilaya ya Monduli,Bw. Shaaban Mngunye (kushoto) akifafanua jambo wa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunde wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa kabla ya kuanza kwa mkutano na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto iliyopo Wilayani humo.
Walimu wa Shule ya Engutoto iliyopo Wilayani Monduli Mkoani Arusha,wakizungumzia changamoto mbali mbali wanazokabiliana nazo katika kazi yao ambapo wengi wamedai kuwa inachangia kwa kiasi fulani kudhorota kwa elimu katika shule hiyo.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimsikiliza kwa makini,Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Shule ya Sekondari ya Engutoto,Bw. Joseph Lukumay.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad