VODACOM TANZANIA YAWAFARIJI WAATHIRIKA WA MAAFA JIJINI DAR ES SALAAM. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


24 Dec 2011

VODACOM TANZANIA YAWAFARIJI WAATHIRIKA WA MAAFA JIJINI DAR ES SALAAM.

Wafanyakazi wa Kampuni ya Vodacom wakishusha sehemu ya magodoro 430 yaliyotolewa na kampuni hiyo katika kambi ya waathirika wa maafa ya Dar es salaam ya Mchikichini. Vodacom iligawa pia mablanketi 480 na vyakula vyote vikiwa na thamani shilingi 30 milioni kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa Vodacom Foundation.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Sadiq Meck Sadick ksuhoto akiwa na Mbunge wa Kinondoni Bw. Iddi Azan akipokea magodoro kutoka kwa Mkuu wa Vodacom Foundation Bw. Yessaya Mwakifulefule .Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja cha Vodacom Bi. Najengwa Mbagga. Vodacom imekabidhi magodoro 430, mablanketi 480 na vyakula vyote vikiwa na thamani ya Shilingi 30 milioni kusaidia kambi za waathirika wa maafa ya Dar es salaam.
Sehemu ya shehena ya magodoro 430 yaliyotolewa msaada na Vodacom kwa waathirika wa maafa ya Dar es salaam yakiwa tayari kukabdhiwa kwa kamati ya maafa ya mkoa wa Dar es salaam. Mbali na magodoro Vodacom ilikabidhi pia mablanketi 480 na vyakula vyote vikiwa na thamani shilingi 30 milioni kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa Vodacom Foundation.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad