Vodacom Miss Tanzania 2011 wapewa semina juu ya M- Pesa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Aug 2011

Vodacom Miss Tanzania 2011 wapewa semina juu ya M- Pesa


Baadhi ya washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakijisajili katika huduma ya M Pesa baada ya kupata semina juu ya faida na umuhimu wa kuwa umejisajili katika huduma hiyo jana wakiwa Kambini katika Jumba la Vodacom. 
Meneja Huduma wa Bidhaa za Vodacom, Elihuruma Ngowi akifafanua jambo juu ya huduma ya M Pesa kwa washiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011 katika kambi yao iliyopo jumba la Vodacom jijini Dar es Salaam jana. 
Baadhi ya washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakipiga picha na mabaunsa waliovalia vazi la M Pesa “m pesa Man” baada ya warembo hao na wenzao kupata semina juu ya faida na umuhimu wa kuwa umejisajili katika huduma ya M Pesa jana wakiwa Kambini katika Jumba la Vodacom. 
Washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakipiga picha na mabaunsa waliovalia vazi la M Pesa “m pesa Man” baada ya warembo hao na wenzao kupata semina juu ya faida na umuhimu wa kuwa umejisajili katika huduma ya M Pesa jana wakiwa Kambini katika Jumba la Vodacom.
Afisa Utawala wa Huduma ya M Pesa kutoka Vodacom, Emmanuel Pallangyo akigawa viperushi vilivyo na maelezo ya namna huduma ya M Pesa kwa washiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011 katika kambi yao iliyopo jumba la Vodacom jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Mpigapicha wetu).

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad