Ukame Kenya Waturkana 14 wafa kwa njaa.... - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

Saturday, 6 August 2011

Ukame Kenya Waturkana 14 wafa kwa njaa....

Ukame umeathiri raia na wanyama nchini Kenya
Takriban watu 14 wamekufa katika eneo la Kaskazini Mashariki katika eneo la Turkana nchini Kenya, vifo vya kwanza kutokea vinavyohusiana na njaa nchini Kenya katika eneo linalohusiana na ukame.

Mbunge wa Turkana, John Munyes, alisema vifo hivyo vimetokea katika vijiji vitatu baada ya serikali kushindwa kusafirisha chakula kwa ajili ya watu walioathiriwa na ukame.
Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya raia wa Kenya milioni nne wanatishiwa na ukosefu wa chakula katika eneo lilikumbwa na ukame mbaya katika kipindi cha miaka 60.
Nchi nyingine zilizoathiriwa ni Somalia, Ethiopia na Djiblouti.
Mwandishi wa BBC Odiambo Joseph akiwa Turkana anasema ametembelea kijiji ambacho mamia ya watu wengi wao wakiwa wazee na dhaifu walikuwa kwenye mstri mrefu wa kugawiwa chakula.
Watu 14 waliokufa nchini Kenya walikuwa watu wazima, lakini watoto pia wana utapiamlo mkali, mwandishi wa BBC anasema.

Maandishi na: Odiambo Joseph BBC

No comments:

Post a Comment