Habari na Matukio : Wanahabari Wahimizwa Kuwasilisha Masuala Yahusuyo Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Magumu, Jijini Arusha - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Jan 2015

Habari na Matukio : Wanahabari Wahimizwa Kuwasilisha Masuala Yahusuyo Watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Magumu, Jijini Arusha


SAM_0767Meneja wa ushirikiano wa The Foundation For Tomorrow Bw.Anton Asukile akiwa anatoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari katika semina ya siku moja juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo  kwa waandishi wa habari Mkoa wa Arusha iliyofanyika katika ukumbi wa Olasiti Garden jijini Arusha
SAM_0747
Mwezeshaji wa Semina juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU Bw.Zachariah A.Babu akiwa anatoa maelekezo kwa waandishi wa habari juu ya Haki ya watoto
SAM_0772Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep akiongea katika warsha juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo.
SAM_0742Waandishi wakiwa wanafatilia sema juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la The Foundation For Tomorrow kulia ni Daniel Lucas mhariri wa Safina Redio na Merry Mwita kutoka gazeti la Mtanzania
SAM_0749 Kulia ni Queen Lema wa gazeti la Majira,Rose Jackson wa gazeti la jambo leo wakiwa katika semina hiyo
SAM_0743Waandishi kutoka Habari Maalum Media Arusha,kulia ni Daniel Magulu na Edith Laizer
SAM_0768Kushoto ni Jamillah Omar wa chanel Ten katikati Happy Lazaro wa mwananchi na Cynthia Mwilolezi wa gazeti la Nipashe
SAM_0770Kushoto Lilian Joel wa gazeti la Uhuru na Elia Mbonea wa gazeti la Mtanzania
SAM_0761Mwezeshaji wa Semina juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU Bw.Zachariah A.Babu akiwa anasisitiza jambo
SAM_0787Waandishi mwandamizi Jamillah Omar wa chanel Ten akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0793Mwandishi mwandamizi wa kituo cha Redio 5 David Rwenyagira akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0764Mwandishi kutoka Habari Maalum Bi.Edith Laizer akiwa anachangia katika semina hiyo
SAM_0773Mwandishi mwandamizi Queen Lema wa gazeti la Majira akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0794Mmiliki wa mtandao wa kijamii wa libeneke la kaskazini Woinde Shiza akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0779Mmiliki wa mtandao wa kijamii http://jamiiblog.co.tz/ Pamela Mollel akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0790Mwandishi wa Star TV Magessa Magessa akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0791Mwandishi wa mambo jambo redio Rotilinde Achimpota akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0784Mwandishi Peter Saramba wa Mwananchi akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0783Mwandishi kutoka gazeti la habari Leo Veronica Mheta akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0782Cynthia Mwilolezi wa gazeti la Nipashe akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0775Elia Mbonea kutoka Mtanznia akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0776Rose Jackson wa Jambo Leo akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0777Daniel Lucas mhariri wa Safina Redio akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0788Mwakilishi kutoka Habari Maalum Daniel Magulu akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0785Mwakilishi kutoka Habari Maalum Edith Laizer akiwa anapokea cheti kutoka kwa Meneja wa mafunzo ya walimu wa shirika la The Foundation For Tomorrow Bi.Melissa Queyquep baada ya kuhudhuria semina ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha
SAM_0795Mwenyekiti wa Arusha press club, Claud Gwandu  akitoa neno la shukrani kwa shirika hilo kuandaa semina kama hiyo kwa waandishi wa habari
SAM_0796Picha ya pamoja
Vyombo vya habari nchini vimehimizwa kuwasilisha masuala yanayowahusu watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu. Akizungumza na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali jijini Arusha katika warsha juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoendeshwa na shirika liliso la kiserikali la The Foundation For Tomorrow (TFFT),
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania wa shirika hilo, Bwa. Kennedy Oulu alisema tatizo la watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu nchini Tanzania ni gumu, hivyo vyombo vya habari havina budi kuifahamisha jamii kuhusu hili suala na matatizo yanayowakabili watoto yatima na waishio katika mazingira magumu ili jamii na wadau mbalimbali waweze kushiriki vema katika kukabiliana na tatizo hili.
“Kwa sasa, inakadiriwa kuwa kuna watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu wapatao 1,800,000 hapa Tanzania pekee, huku 1,300,000 kati yao wakiwa wametokana na athari za ugonjwa wa UKIMWI. Mgawanyo wa kifamilia na muundo wa kimsaada kijamii ni moja ya vinavyochangia tatizo hili. Vinapoongezwa katika umaskini unaojidhihirisha katika: ukosefu wa upatikanaji wa huduma za elimu ikiwemo elimu ya awali, ukosefu wa upatikanaji wa huduma za afya na uzalishaji kama afya ya uzazi, ukosefu wa stadi za maisha zinazoakisiwa katika mitaala ya shule zenye uwezo unaotakiwa na ubunifu ili kujenga uwezo wa watoto, si kwa yatima na waishio katika magumu pekee”. Alisema Kennedy na kuongeza
“Ni muhimu kutambua kuwa kumekuwa na hatua na mafanikio yaliyofikiwa na wadau mbalimbali ikiwemo serikali katika kuwezesha upatikanaji, kuzijengea uwezo familia za watoto hawa na kubadili mitazamo ya jamii dhidi ya watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu, hii inajenga msingi wa mwitikio endelevu.
Kwa upande wake, shirika la The Foundation For Tomorrow limekuwa likilishughurikia tatizo hili kwa njia mbalimbali. Shirika hili hutumia njia anuai ambazo hupunguza uhitaji wa watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu kwa kuzijengea uwezo wa kiuchumi kaya zao hususani zile kaya maskini kupindukia, kutoa msaada wa kugharamia masomo ili kuwahakikishia upatikanaji wa elimu, kutoa bima za afya kwa wanafunzi yatima na wale waliotoka katika mazingira magumu, kuwajengea uwezo walimu na kuwezesha stadi za maisha kwa njia ya kuboresha mtaala.
Bwa. Oulu amesema juhudi hizi pamoja na sauti za watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu zinapaswa kufahamika. “Changamoto za hawa watoto na mitazamo yao hutusaidia kutambua njia iliyo bora ya kulinda maisha yao. Hizo pia hutuwezesha kutambua kuwa kwa kiasi kikubwa sote tunalo jukumu la kubadili vile tunavyowachukia hawa watoto kutoka katika kudharauliwa na badala yake kuwa katika ufahamu kuwa sababu ya hali hizo na magumu yaliyopo ndiyo matatizo tunayoyashughurikia Tanzania yote: elimu, afya, umaskini, kaya na kufikia fursa zilizopo.”
Inapaswa kuoneshwa ya kwamba hali hii lazima ionwe kuwa si ya kudumu wakati hatua zinazochukuliwa, kujenga kipato baina ya kaya maskini, kuwezesha upatikanaji wa mahitaji na kulinda haki na ulinzi kwa watoto, hususani kwa kuwahakikishia elimu bora na ushiriki wao usio na kikomo ni muhimu katika kutokomeza tatizo hili.
Bwa. Oulu aliongeza kuwa “Uandishi wa habari wa kiuchunguzi na uwasilishaji mambo wenye malengo, suluhisho, utendaji bora na juhudi zilizoshindwa ndivyo vitaiwezesha jamii kujua ni njia gani bora ya kusaidia, kuitikia na kudumisha juhudi na fursa za kuwaondoa watoto yatima na wale wasiojiweza kutoka katika janga hilo. Inapaswa ioneshwe kuwa watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu pamoja na wanaowahifadhi na kaya zao wanayo hatua kubwa ya kuchukua.”
Sambamba na hilo, msimamizi wa warsha hiyo Bwa. Augustine Zacharia alivishauri pia vyombo vya habari kuzingatia ni jinsi gani habari zinazotolewa katika vyombo vyao huwaathiri watoto hawa kwa upande chanya na hasi. Masuala yahusuyo watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu yanapaswa kuwasilishwa katika namna ambayo huwajenga na kuwa katika mtazamo wa kutafuta suluhisho la tatizo. Licha ya kuwa kuna uhuru wa kutoa na kupokea habari, lakini namna ambavyo habari hizi huwasilishwa, zinapaswa kwanza kuzingatia kuwa haki za watoto hazivunjwi.
*********************************************
KUHUSU THE FOUNDATION FOR TOMORROW.
The Foundation For Tomorrow huutazamia ulimwengu ambao watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu wanachangia katika jamii kama raia waliowezeshwa bila kubaguliwa, kuathiriwa, na uhitaji. Lengo la shirika hili ni kuhakikishia elimu bora na msaada wa kihisia kwa watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu ili waweze kufikia viwango vya juu kabisa vya uwezo wao na kushamiri katika jamii zao. (Habari Picha na Pamela Mollel wa Jamiiblog)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad