Matukio : Kamati ya Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Arusha yaiomba serikali kuboresha Mahabusu ya Watoto ,Jijini Arusha - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Mar 2016

Matukio : Kamati ya Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Arusha yaiomba serikali kuboresha Mahabusu ya Watoto ,Jijini Arusha


Kutoka Kulia Phidesia Mwakitalima,  katibu wa Jumuiya ya wazazi   ccm wilaya Arusha  Rehema mohamed , Augustino Masawe wawakilishi kamati ya utekelezaji wazazi wilaya ya Arusha wakiwa na Afisa ustawi wa jamii jiji la  Arusha  Mussa mkamate katika mazungumzo juu ya Mahabusu ya watoto Arusha.


picha ikionyesha uchakavu wa vyoo vya mahabusu ya watoto Arusha pamoja na pakti za viroba ambavyo wanakunywa kisiri  siri na kuletewa kinyemela na vijana wa mtaani kutokana na kukosa ulinzi  kwa mahabusu hayo pia kukosekana kwa uzio katika magereza hiyo ya watoto , na imeonekana pia kuna matundu ya mapaa  ya mabati ambayo ayapo pichani Matundu ambayo yamechakaa yanatumika na watoto hao kama  njia ya kutorokea nje ambapo  mara kadhaa  hukamatwa wakiwa wanatoroka na kurudishwa ndani


Na Woinde Shizza,Arusha

Kamati ya utekelezaji Jumuia ya wazazi wilaya ya Arusha  inatarajia kutembelea  mahabusu ya watoto Arusha  katika kuazimisha sherehe ya wiki ya wazazi Tanzania inayofanyika kila april 2 kila mwaka .

Katika maazimisho hayo pia kamati hiyo imejipanga kukarabati baadhi ya miundo mbinu ya kituo cha mahabusu ya watoto iliyopo jijini hapa .
Akizungumzia maadhimisho hayo katibu wa jumuiya ya wazazi  CCM wilaya ya Arusha  Rehema Mohamed alisema  wao kama wazazi wamegundua kuna changamoto nyingi katika mahabusu ya watoto mkoani Arusha ambazo wazazi kama walezi wameona ni vyema kutembelea mahabusu ya watoto kuwaona    na kuwapelekea chochote kinachopatikana .

Alisema kuwa wanajaribu pia  kutatua changamoto nyingi wanazokabiliana nazo ili kuweza kuwasaidia watoto hao nao waishi kama watoto wengine walioko majumbani .

 “kwa kweli natoa wito kwa wazazi wote watakaoguswa Arusha kujumuika nasi tar 2 mwezi wa nne kuanzia saa 3kamili asubuhi  kwani watoto wengine wazazi wao wamewatelekeza kabisa na wengine hawana wazazi kabisa”alisema  Rehema  
Kwa upande wake  mjumbe wa Kamati hiyo  Phidesia  Mwakitalima alisema kuwa Watoto hawa wengine wazazi wao hawaji kuwaona wengine hawana wazazi wanakabiliana na changamoto nyingi sana ikiwemo pia kesi zao kwenda taratibu.


Mwakitalima alisema   kwa sababu watoto waliopo katika mahabusu hiyo  ni watoto wenye  haki ya kupata elimu  hivyo pia aliomba serekali ijaribu kuwafikiria watoto hawa ambao wapo mahabusu .
Ameongeza kuwa endapo watoto hao watapatiwa elimu wakiwemo mahabusu  itawasaida kwani hata wakiondoka hapo hawataondoka bure  na pia atatoka na elimu ambayo itamsaidia ata akienda kuondoa ujinga mtaani na pia itamsaidia ata kutoweza kujiingiza katika makundi mabaya ya mtaani kwani atakuwa na elimu kidogo ambayo itamsaida katika maisha yake.

 Aidha aliomba serekali pia iangalie mahabusu hiyo kwani  watoto wengine kesi zao zinasikilizwa mda mrefu bila suluhu na makosa mengine kisheria likifikishwa mahakamani kesi inapaswa kuisha siku hiyo hiyo

“mfano hapa kuna kesi ya mauaji mtoto alimsaidia dada yake asichomwe kisu na shemeji yake akachukua kisu akamuwahi shemeji yake na amekubali kosa lakini mwaka wa pili mahakamani wanasema ushahidi haujakamilika hivyo jamani naomba serekali iangalie sana hawa watoto kwani mbali na yote wanateseka wasaidie angalau kesi zao zisikilizwe kwa wakati na watendewe haki jamani kiukweli inauma naomba  serekali iwaangalie awa watoto jamani “alisema Phidesia  

Aidha aliomba serekali kuangalia kwa makini sana mahabusu hii ya  watoto kwani mbali na hivi pia mahabusu hii watoto wakiumwa wanapelekwa hospital na pikipiki hakuna gari ya mahabusu saa nyingine dawa zinakosekana na maafisa kujikuta wakijipapasa mifukoni mwao kunusuru watoto umauti usiwakute.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad