Matukio : Katibu Mkuu wizara ya ujenzi aipongeza JICA kwa Ufadhili wa Miradi Mbali mbali ya Barabara Nchini - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

Thursday 19 March 2015

Matukio : Katibu Mkuu wizara ya ujenzi aipongeza JICA kwa Ufadhili wa Miradi Mbali mbali ya Barabara Nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe (kushoto), akimkabidhi zawadi Mwakilishi Mkuu mpya wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) Toshio Nagase (kulia) Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe akifurahi jambo na Ujumbe kutoka wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) wakati ugeni huo ulipotembelea ofisini kwake kwa lengo la kutoa pongezi za JICA kwa Wizara ya Ujenzi kutokana na utekelezaji mzuri wa miundombinu ya barabara.Picha na Habari kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe amelipongeza Shirika la Misaada ya Maendeleo la Japan (JICA) kwa ufadhili wa miradi mingi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara iliyokamilika na inayoendelea nchini.

Eng. Iyombe ametoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam wakati akiagana na Mwakilishi Mkuu wa JICA nchini Bw. Yasunori Onishi, ambae amemaliza muda wake na kumpisha Mwakilishi Mkuu mwingine Bw. Toshio Nagase.

“Nafikiri ninyi ni wa kwanza kufadhili miradi mingi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara nchini kwetu, kwani mmekuwa mkiahidi kufanya mambo mazuri na kuyatekeleza kwa kipindi kifupi, hivyo sina budi kuwashukuru kwa jitihada hizi”, alisema Eng. Iyombe.

Katibu Mkuu ameongeza kuwa miradi mingi ya barabara ambayo inafadhiliwa na JICA inaonekana kukamilika kwa wakati hivyo kutoa fursa za kimaendeleo nchini.

Aidha, Eng. Iyombe amefafanua kuwa Wizara ya Ujenzi itaendelea kushirikiana kwa karibu na Shirika la JICA ili kuhakikisha miradi yote ambayo wameiahidi kuitekeleza inafanyika na kumalizika kwa wakati. Awali, akimkaribisha Mwakilishi Mkuu Mpya wa JICA nchini Bw. Toshio Nagase, Katibu Mkuu ameahidi kuwa Wizara ya Ujenzi itatoa ushirikiano wa karibu kwake kama ilivyokuwa inafanya kwa mtangulizi wake.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkuu wa JICA nchini aliyemaliza muda wake Yasunori Onishi, amesema kuwa furaha yake ni kuona Tanzania inakuwa na miundombinu bora katika ya sekta ya barabara ambapo amesisitiza kuwa Shirika hilo linajikita katika kuhakikisha kuwa inajenga na kukarabati barabara za miji, mikoa na zile zinazounganisha nchi.

Zaidi ya miradi 26 ya barabara nchini imefadhiliwa na Shirika la maendeleo la Japan (JICA) tangu mwaka 1980 hadi sasa, lengo likiwa ni kupunguza msongamano na kuhuisha fursa za kiuchumi.

Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa daraja la Selander, ukarabati wa barabara ya Makuyuni – Ngorongoro pamoja na ukarabati wa barabara ya TANZAM katika eneo la Kitonga, ujenzi wa barabara ya Masasi- Mangaka, Upanuzi wa barabara ya Bagamoyo eneo la Mwenge – Tegeta, ujenzi wa daraja la Rusumo ambayo yote imekamilika.

Miradi mingine inayotarajiwa kuanza kujengwa muda wowote ni upanuzi wa barabara ya Gerezani, ujenzi wa barabara za juu (Tazara flyovers), na ujenzi wa barabara ya Morocco- Mwenge itakayojengwa kwa njia nne.

No comments:

Post a Comment