DR. SHEIN AZUNGUMZA NA WANAFUNZI NCHINI CHINA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


31 May 2013

DR. SHEIN AZUNGUMZA NA WANAFUNZI NCHINI CHINA

IMG_2467Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Elimu za Juu katika Vyuo Vikuu katika Mji wa Nanjing Jimbo la Jiangsu nchini China,wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Sofitel Luxury Hotel,katika mazungumzo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein. IMG_2467Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Elimu za Juu katika Vyuo Vikuu katika Mji wa Nanjing Jimbo la Jiangsu nchini China,wakisikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) wakati alipozungumza nao katika ukumbi wa mikutano wa  Sofitel Luxury Hotel, Mjini Nanjing katika jimbo la Jiangsu akiwa katika ziara  ya Kiserikali. IMG_2482Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kushoto) akiwa na Mama Mwanamwema Shein,kushoto pamoja na Mawaziri na Maofisa aliofuatana nao katika ziara ya Kiserikali nchini China,Rais alipata muda wa kuzungumza na wanafunzi wa Tanzania wanaosoma  katika Vyuo Vikuu mbali mbali, na  aliwaelezea  hali halisi ya Utulivu na Amani Iliyopo nchini Tanzania  ambapo aliwataka kuondokana na wasiwasi. IMG_2487Mwanafunzi Sauli Elingarama ,Dkt wa Binadamu aliokuwa akiuliza swali mbele ya Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,wakati wa mazungumzo na Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Vyuo Vikuu vya Mji wa  Nanjing Nchini China katika jimbo la Jiangsu,Rais yupo  China kwa ziara ya kiserikali.Picha na Ramadhan Othman China.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad