Matukio : Rais Jakaya Kikwete Apokea Hati ya Utambulisho wa Balozi wa Denmark Nchini - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


22 Aug 2015

Matukio : Rais Jakaya Kikwete Apokea Hati ya Utambulisho wa Balozi wa Denmark Nchini

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto) akipokea hati ya utambulisho ya Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kulia) Ikulu jijini Dar es salaam wakati alipokwenda kujitambulisha.
Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen akisaini kitabu cha wageni wakati alipokuwa anaenda kukabidhi hati ya utambulisho na kujitambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kulia) wakati alipokwenda kujitambulisha na kukabidhi hati ya utambulisho Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kulia) akisalimiana na Balozi wa Denmark (kushoto) nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen mara baada ya kukabidhi hati ya utambulisho Ikulu jijini Dar es salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kulia) akibadilishana mawazo na Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kushoto) wakati alipokwenda kujitambulisha na kukabidhi hati ya utambulisho Ikulu jijini Dar es salaam.
Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (kulia) akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Maadhi Juma Maalimu (wa pili kushoto) Ikulu jijini Dar es salaam.
Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (katikati mstari wa mbele) akiwa amesimama wakati nyimbo za taifa za Tanzania na Denmark zikiimbwa Ikulu jijini Dar es salaam alipokwenda kujitambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
 Bendi ya Jeshi la Polisi nchini ikipiga nyimbo za taifa za Tanzania na Denmark wakati Balozi wa Denmark nchini Tamzania Einar Hebogard Jensen (katikati mstari wa mbele) alipokuwa anakwenda kujitambulisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad