Mratibu
Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akisalimiana na Mwandishi
mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog,
Andrew Chale alipotembelea katika banda la mtandao huo ambao mwaka huu
mwezi Septemba unatimiza miaka 7 tangu kuanzishwa ambapo wametumia fursa
ya maonyesho ya saba saba kukutana na wadau mbalimbali wanaotumia
mtandao huo kupata habari mbalimbali sambamba na kubadilishana mawazo na
ushauri wa maboresho ya kazi. Kushoto aliyefuatana naye ni Mtaalam wa
Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu.
Kulia ni mdau wa karibu na mshauri wa mtandao wa habari Modewjiblog,
Lemmy Hipolite.
Mratibu
Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, aliyeambatana na Mtaalam wa
Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu
akiangalia moja ya documentary ya TV katika banda hilo minayoonyesha
wadau mbalimbali wanaotumia mtandao huu ambao walipata kuhojiwa.
Mmoja wa wadau wa Modewjiblog, Rehema
Pascal akiuzungumzia mtandao wa habari wa Modewjiblog alipotembelewa
ofisini kwake wakati wa kurekodi 'documentary' hiyo.
Pichani
juu na chini ni Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akiangalia kazi mbalimbali zinazofanywa kwenye mtandao wa habari wa Modewjiblog alipotembelea banda
hilo katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba
yanaoendelea kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya
Kilwa, jijini Dar.
Mratibu
Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiondoka mara baada ya
kutembelea banda la Modewjiblog, lililopo katika banda la MeTL Group.
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa Modewjiblog,
Zainul Mzige akitoa maelezo juu ya mtandao huo unavyofanya kazi zake
ambapo aliwataka vijana hao kutembelea mara kwa mara ikiwemo kufaidika
na nafasi za ajira zinazotolewa kwenye mtandao huo zikiwemo habari za
kitaifa na kimataifa, burudani, michezo, utamaduni n.k.
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige (kulia) na Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog,
Andrew Chale wakikabidhi zawadi za fulana maalum kwa wadau
waliotembelea katika banda la mtandao huo katika maonyesho ya 39 ya
kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea kurindima katika viwanja vya
Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale akikabidhi zawadi ya kofia na fulana kwa Mmiliki wa blog ya Kajunason blog, Cathbert Kajuna (kulia) aliyetembelea banda la mtandao huo.
Wadau wakiendelea kumiminika kwenye banda la Modewjiblog katika
maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara Sabasaba yanaoendelea
kurindima katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini
Dar.
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale akikabidhi zawadi ya fulana na kofia kwa Mwandishi wa Michuzi blog, Chalila Kibuda aliyembelea banda hilo.
Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog,
Andrew Chale (kulia) akitoa maelezo ya utofauti wa habari za kwenye
magazeti na blog kwa mmoja wa wadau anayesoma habari mbalimbali
katika mtandao huo, Peter Chilumba.
No comments:
Post a Comment