Matukio/Siasa :Mgombea Ubunge Jimbo la Arusha Mustafa Panju Awataka Wananchi Kukataa Rushwa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


29 Jul 2015

Matukio/Siasa :Mgombea Ubunge Jimbo la Arusha Mustafa Panju Awataka Wananchi Kukataa Rushwa


Mkurugenzi wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ubunge wa jimbo la Arusha kwa tiketi ya CCM akinadi sera zake mbele yawananchi na wanachama wa chama hicho katika kata ya Moivaro ofisi za kata hiyo jijini Arusha ili kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea wa ubunge jimbo la Arusha kupitia CCM,aliwataka watanzania kuiga nyendo za Baba wa Taifa Mwalimu Julias Nyerere kwa kuwa na upendo,ushirikiano na kukataa rushwa(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_4457Mkurugenzi wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ubunge wa jimbo la Arusha kwa tiketi ya CCM akicheza wimbo wa chama cha mapinduzi ,...CCM MBELE KWA MBELEEEEEEEEE ......kushoto kwake ni Mtia nia mwenzake wakili msomi Edimond Ngemela na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Monaban yajijini Arusha,Philemon Mollel ambaye pia ni Mgombea Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM
SAM_4442 Mosses Mwizarubi ambaye pia ni mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM akiomba ridhaa kwa wananchi pamoja na wananchama wa chama hicho kuwatumikia katika nafasi ya Ubunge
SAM_4452Mkurugenzi wa Bushback Safaris Mustafa Panju akimwaga sera zake mbele yawananchi na wanachama wa chama hicho katika kata Olorieni katika uwanja wa ccm,alisisitiza watu kujitolea kwa upendo kama alivyofanya Baba wa Taifa hili Mwalimu Jualias Nyerere kwa kusimamia na kuweza kukomboa Nchi na hakukuwepo na swala la rushwa
SAM_4456 Wakili msomi Edimond Ngemela anayeomba ridhaa ya ccm katika nafasi ya ubunge akisalimiana na mmoja wa wananchi waliojitokeza kuwasikiliza watia nia kupitia chama cha mapinduzi CCM katika kata ya Olorieni jijini Arusha
SAM_4447Mohamed Omary ambaye pia ni mgomea Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM akimwaga sera zake ambapo alisema kuwa akipata ridhaa ya kuwatumikia atahakikisha anawachukulia hatua kali wale wote wanaotelekeza watoto hali inayosababisha watoto wa mtaani kuongezeka
SAM_4459Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano ambaye pia ni msimamizi wa uchaguzi akiongea katika mkutano huo
SAM_4469Katibu wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano ambaye pia ni msimamizi wa uchaguzi kulia akiwa na mmoja wa wagombea mapindizi Mosses Mwizarubi
SAM_4485Mtia nia ya Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM Thomas Munisi akimwaga sera zake katika kata ya Moivaro akiomba ridhaa ya kwa wananchi ya kuwatumikia katika nafasi ya ubunge jimbo la Arusha mjini
SAM_4476
Taswira katika kata ya Moivaro jijini Arusha

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad