Maisha Yetu : Idara ya Uhamiaji Yatoa Msaada kwa Watoto Yatima Wilayani Makete, Mkoani Njombe - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


17 Dec 2014

Maisha Yetu : Idara ya Uhamiaji Yatoa Msaada kwa Watoto Yatima Wilayani Makete, Mkoani Njombe


 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro (kushoto) na afisa uhamiaji mkoa wa Njombe Rose Mhagama wakiwa kituoni hapo.
 Afisa uhamiaji mkoa wa Njombe Rose Mhagama akiwa amembeba mtoto yatima anayelelewa kituo cha Nyumba ya yatima Bulongwa
 Mkuu wa wilaya akifurahia jambo
 Watoto yatima wakipewa zawadi na Idara ya uhamiaji mkoa wa Njombe
Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akiwa amembeba mtoto yatima anayelelewa kituo cha Nyumba ya yatima Bulongwa
 
 Baadhi ya msaada uliotolewa
 Mkuu wa wilaya akikabidhiwa msaada huo na afisa uhamiaji mkoa wa Njombe
 
 Afisa Uhamiaji mkoa wa Njombe akisema mawili matatu
 akiwa kwenye picha ya pamoja na watoto yatima 
 Mkuu wa wilaya katika picha ya pamoja na watoto yatima
Hivi karibuni Idara ya uhamiaji mkoa wa Njombe iliunga mkono jitihada za mkuu wa wilaya ya makete Josephine Matiro kusaidia vituo vya watoto yatima wilayani humo kwa kutoa msaada wa zaidi ya shilingi milioni 1

Akizungumza wakati akikabidhi msaada wao afisa uhamiaji mkoa wa Njombe Rose Mhagama alisema wameguswa na suala hilo na kuamua kuvisaidia vituo vya watoto yatima Makete vitu mbalimbali, na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuwasaidia watoto hao

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya Hiyo Bi Josephine matiro amewataka wanamakete kubadilika na kuacha dhana kuwa watoto hao watasaidiwa na wafadhili kutoka nje na badala yake nao wawasaidie watoto hao kwa kitu chochote walichojaliwa na Mungu

Vituo vilivyonufaika ni Nyumba ya yatima Bulongwa, Fema Matamba na Kituo kipya cha Kisinga

Na Edwin Moshi wa eddy blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad