Miundo Mbinu Zetu :Hii ndio Barabara Iliyokarabatiwa kwa Milioni 90 Ukonga Mazizini - Moshi Bar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


10 Nov 2014

Miundo Mbinu Zetu :Hii ndio Barabara Iliyokarabatiwa kwa Milioni 90 Ukonga Mazizini - Moshi Bar


 Hii ndio ile barabara ya Ukonga Mazizini- Moshi Bar ambayo inadaiwa kugharimu kiasi cha shilingi Milioni 90 kuikarabati kwa kiwango cha changarawe kwa umbali wa kilometa tatu. Picha hizi ni madimbwi ya mwanzo tu ya hizo kilometa tatu.
Meya Jerry Silaa wa Ilala ambaye ni Diwani wa Gongo la Mboto alipotembelea aliwaambia wananchi kuwa fedha za ujenzi huo ni kutoka mfuko wao ni . PICHA ZA CHINI NI SIKU MEYA SILAA ALIPOTEMBELEA UJENZI WAKE. 


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa Jana amefanya ziara fundi ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya ukonga Moshibarkilometa 3 kiwango cha changalawe awamu yakwanza. Ikiwa ni utekelezaji wa miradi yadharura kulingana na uharibifu wa miundo mbinuulitokea baada ya Mvua kubwa. Mradi huoambao unaghalimu kiasi cha shilingi millioni 90.Pesa za Ujenzi huohizo zinatoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.Pia Barabara hiyo itawekwa Lami kwa awamu ya pili ndani ya mwaka huu kwa kilomita tatu.
Greda likirekebisha Barabara ya Ukonga-mazizini kulekea moshi bar
Mwonekano wa Bara barabara hiyo. Picha na Father Kidevu Blog.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad