Mwenyekiti
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Zitto Kabwe
akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini,Mhe. Ismail Aden Rage
wakati akiwasili bungeni kuwasilisha Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za
Serikali kuhusu akauti ya ESCROW.
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anne Makinda akifafanua
jambo wakati akiendesha Bunge hilo mjini Dodoma.
Mwenyekiti
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Zitto Kabwe
akienda kusoma Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kuhusu akauti ya ESCROW.
Mwenyekiti
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mhe Zitto Kabwe
akisoma Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kuhusu akauti ya
ESCROW Bungeni Mjini Dodoma.
Waheshimiwa Wabunge wakimsikiliza Mhe. Zitto Kabwe (hayupo pichani) wakati akisoma ripoti ya Mkaguzi wa hesabu za serikali Bungeni.
Baadhi ya wahudumu wa Bunge wakigawa Ripoti ya hiyo kuhusu akauti ya ESCROW kwa Wabunge
Waheshimiwa
Wabunge wakipitia ripoti hiyo kwa makini wakati ikisomwa na
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Mhe Zitto
Kabwe.
Baadhi ya waandishi wanaoripoti habari za Bunge wakifuatilia mjadala kwa makini.
Naibu katibu wa Bunge, John Joel akijadiliana jambo na Mhe. Spika Anna Makinda.
Wabunge wakiwa wamesimama kuashiria kuunga mkono taarifa iliyosomwa Bungeni na Mhe. Zitto Kabwe.
Mhe Said Arfi akimpongeza Mhe.Zitto Kabwe ,mara Baada ya kumaliza kusoma ripoti hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Deo Filikunjombe akiwasilisha maazimio ya kamati yake.
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anne Makinda akitoka
ndani ya Ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirisha Bunge mpaka tarehe 27 Novemba 2014
ambapo Serikali inatarajiwa kutoa majibu.
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini,Mhe. Stephen Masele akizungumza na waandishi
wa habari mara baada ya Bunge kuahirishwa. Picha zote na Deusdedit
Moshi
No comments:
Post a Comment