MATUKIO : TASWIRA YA MSANII TOKA MAREKANI T.I ALIVYOPEWA ZAWADI YA PICHA, JIJINI DAR ES SALAAM - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


22 Oct 2014

MATUKIO : TASWIRA YA MSANII TOKA MAREKANI T.I ALIVYOPEWA ZAWADI YA PICHA, JIJINI DAR ES SALAAM


Msanii TI akiingia katika Ukumbi wa Bongoyo uliopo katika Hoteli ya Sea Cliff Jijini Dar Es Salaam kwaajili ya kufanya mkutano na waandishi wa Habari kabla ya kupanda kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Bw Steve Ganon akiongea na wanahabari katika ukumbi wa mikutano wa Bongoyo uliopo katika Hoteli ya Sea Cliff Jijini Dar wakati timu nzima ya Serengeti na Prime Time Promotions ambao ndio waandaaji wa Tamasha la Fiesta walipokuwa wakimtambulisha msanii nguli kutoka Nchini Marekani TI kabla ya kupanda jukwaani katika Viwanja vya Leaders.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Bw Joseph Kusaga akitoa machache kabla ya kumtambulisha Msanii wa Muziki Kutoka Nchini Marekani TI ambae atapanda kwenye jukwaa la Fiesta katika Viwanja vya Leaders.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Ephraim Mafuru akitoa machache wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar Es Salaam.
Baadhi ya wasanii kutoka mataifa mbalimbali ambao watapanda katika jukwaa la Serengeti Fiesta
Msanii kutoka nchini Nigeria Davido akiongelea jinsi atakavyo wapagawisha watanzania leo katika jukwaa la Serengeti Fiesta muda mchache ujao katika viwanja vya Leaders.
 Kijana wa Kitanzania ambae amemchora TI katika taswira ya Kimasai na kumkabidhi msanii TI kama Zawadi kutoka Tanzania
Wanahabari wakiwajibika wakati wa mkutano wa Kumtambulisha Msanii TI ambae atapanda katika jukwaa la Serengeti Fiesta katika Viwanja vya Leaders.Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad