MICHEZO YETU :Wanamichezo wa Tanzania warejea huku wakiijengea nchi heshima ya kuwa na nidhamu - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


7 Aug 2014

MICHEZO YETU :Wanamichezo wa Tanzania warejea huku wakiijengea nchi heshima ya kuwa na nidhamu


Mwakilishi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko (kushoto) akisalimiana na baadhi ya Wanamichezo waliokuwa kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland mara walipowasilia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Juliana Yassoda akiwaelekeza jambo baadhi ya Wanamichezo waliwakirisha Tanzania kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland mara walipowasilia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Bw. Filbert Bayi akifurahia jambo na baadhi ya wanamichezo walikuwa wamewakilisha nchini katika mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Hermas Mwansoko Akizungumza kwa niaba ya Serikali na wanamichezo waliokuwa kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland mara wakati wa hafla fupi ya mapokezi iliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jan.Kulia ni Katibu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Bw. Filbert Bayi.
Katibu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Bw. Filbert Bayi akizungumza na wanamichezo waliokuwa kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland wakati wa hafla fupi ya mapokezi iliyofanyika jana katika Ukumbi uliopo Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.wa tatu kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Bibi. Juliana Yassoda na Meneja wa Uwanja wa Taifa Bw. Rish Urio.
Mwakilishi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Profesa Hermas Mwansoko akikabidhiwa Bendera ya Taifa na Kapteni wa Timu ya Taifa iliyoshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola Bw. Seleman Kidunda, mara baada ya kurejea nchini. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Bibi. Juliana Yassoda, Meneja wa Timu hiyo Muharami Mchume na Katibu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Bw. Filbert Bayi.
Baadhi ya wanamichezo walioshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland, wakiwa nje ya uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere mara baada ya kuwasili nchini.
Baadhi ya wanamichezo walioshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow Scotland, wakifuatilia hotuba kutoka kwa viongozi mbalimbali (hawapo pichani)wakati wa hafla fupi ya mapokezi na kuwakaribisha iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA FRANK SHIJA.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad