MICHEZO : TANZANIA INAHITAJI UWANJA KAMA HUU ILI TUPATE KOMBE KWA KILA MCHEZO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


21 Aug 2014

MICHEZO : TANZANIA INAHITAJI UWANJA KAMA HUU ILI TUPATE KOMBE KWA KILA MCHEZO


Ili nchi yetu iondokane na aibu inayosababishwa na wachache ni sharti sasa wananchi tukubali kuishauri serikali iwekeze katika ujenzi wa KITUO CHA TAIFA CHA MICHEZO. Kituo ambacho kitanufaisha vipaji vya michezo yote bila kubagua, kituo ambacho kitakuwa ‘Kiwanda cha Kuibua Vipaji vya kuiletea nchi sifa.
Tangu mwaka 2006 wadau tulifanya juhudi za kupeleka mipango yetu serikalini ili wahusika wa maswala ya michezo wapate kushauriana nasi jinsi ya kutatua tatizo sugu ambalo linaikumba nchi yetu. Mifano ya (ramani na picha) hizo zilikuwa zikitupiwa kapuni ili "Bwana Mkubwa" asione.
'Hatimaye mapema mwaka huu idea zetu hizi zilifika kwa wahusika wa juu kabisa na hatua za IMPLEMENTATION zimeanza kwa amani na uzalendo usiokuwa na kipimo'

Wadau wazalendo tunaomba mawazo na ushauri zaidi ili mwisho wa siku Tanzania yetu ifikie hatua ya kutabasamu pindi timu zetu zinaporejea nyumbani kutoka kwenye viwanja vikubwa vya dunia. CHANZO : Gidabuday Blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad