UTALII NA MATUKIO : TANAPA YAWAKUTANISHA WADAU WA HIFADHI MOROGORO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


26 Jul 2014

UTALII NA MATUKIO : TANAPA YAWAKUTANISHA WADAU WA HIFADHI MOROGORO


Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa, (TANAPA) Allan Kijazi akitoa salamu zake wakati wa ufunguzi wa Warsha ya  Mashirikiano kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa mikoa inayopakana na Hifadhi za Taifa. Mkutano unaofanyika katika Hoteli ya Nashera mkoani Morogoro.
Mmoja wa washiriki katika Warsha ya Mashirikiano baina ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama na TANAPA,  Mrakibu wa Polisi, Mary Lugola akitoa neno la shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera mara baada ya kufungua warsha ya viongozi hao .
Baadhi ya washiriki katika warsha hiyo wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera alipokuwa akifungua warsha hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali vya habari nchini wakichukua matukio muhimu wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Udzungwa, Vitalis Uruka akitoa mada juu ya Changamaoto za Uhifadhi katika Kanda ya Kusini na hali halisi.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire Stephen Qoli akitoa mada juu ya Changamaoto za Uhifadhi katika Kanda ya Kaskazini na hali halisi.
Meneja Mawasiliano, TANAPA Pascal Shelutete akitoa mada ya Utaratibu wa kutoa Taarifa kwa Umma juu ya masuala ya Ulinzi na Usalama wa Maliasili na Watalii.
Mshiriki wa warsha hiyo, Franco Kibona akichangia mada katika warsha hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Elias Tarimo akichangia mada wakati wa warsha hiyo.
Mshiriki Abdulla Suleiman akichangia mada katika warsha hiyo.
Mshiriki Faustine Masalu akichangia mada katika warsha hiyo.
Mkurugenzi Mkuu TANAPA, Allan Kijazi akichagia mada katika warsha hiyo.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa katika picha ya pamoja.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA, Allan Kijazi pamoja na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP, Leonard Paul mara baada ya ufunguzi wa warsha hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad