MUZIKI WETU :THT YAANDAA HAFLA YA KUMUAGA MSANII LINAH KWENDA (NO FAKE ZONE) JIJINI DAR - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


17 Jul 2014

MUZIKI WETU :THT YAANDAA HAFLA YA KUMUAGA MSANII LINAH KWENDA (NO FAKE ZONE) JIJINI DAR


 Mkurugenzi wa Tanzania House Of Talent (THT) Ruge Mutahaba akiongea katika halfa ya kumuaga msanii Linah jana Julai 16, 2014 kutoka kwao na kuelekea kampuni ya No Fake Zone (NFZ) ambao ndiyo wanaanza kumsimamia msanii huyo.

 Mkurugenzi wa THT, Ruge Mutahaba akigawa cheti cha ustadi wa kazi wa Msanii Mwasiti ambaye ameitambulisha vyema taasisi yao tokea imenza.
Mtayarishaji wa Muziki Emma The Boy akiurahia jambo mara baada ya kupokea cheti chake cha ustadi bora wa kazi.
  Mkurugenzi wa THT, Ruge Mutahaba akimpa zawadi ya cheti cha ustadi wa kazi wa Msanii Ditto ambaye ameitambulisha vyema taasisi yao tokea imenza.
Msanii Ditto akifurahia cheti chake cha ustadi wa kazi.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya FNZ, Abby akiongea machache wakati wa hafla ya kukabidhiwa rasmi msanii Linah ili waweze kumsimamia kazi zake. Hafla hiyo ilifanyika Julai 16, 2014 ndani ya ofisi za THT jijini Dar es Salaam.
 Msanii Linah akitoa shukrani zake kwa THT kwa jinsi walivyomlea tokea amejiunga mwaka 2009 na mpaka leo ameondoka. Pembeni ni Mkurugenzi wa Kampuni ya FNZ, Abby ambaye ndiye anayemchukua msanii huyo kumsimamia kazi zake. Hafla ya kumuaga Msanii huyo ilifanyika Julai 16, 2014 ndani ya ofisi za THT jijini Dar es Salaam
  Msanii Linah akitoa zawadi kwa Mkurugenzi wa THT, Ruge Mutahaba katika hafla ya kumuaga Msanii huyo ilifanyika Julai 16, 2014 ndani ya ofisi za THT jijini Dar es Salaam
   Msanii Linah akitoa zawadi kwa Mwalimu wake Nkya ambaye alikuwa msitari wa mbele kumuongoza mpaka leo amefanikiwa katika hafla ya kumuaga Msanii huyo ilifanyika Julai 16, 2014 ndani ya ofisi za THT jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad