UCHUMI NA BIASHARA : SERIKALI INATARAJIA KUFUFUA KIWANDA CHA MATAIRI CHA GENERAL TYRE KILICHOPO NJIRO ,JIJINI ARUSHA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Mar 2014

UCHUMI NA BIASHARA : SERIKALI INATARAJIA KUFUFUA KIWANDA CHA MATAIRI CHA GENERAL TYRE KILICHOPO NJIRO ,JIJINI ARUSHA

Timu ya wakaguzi wa miradi wa maendeleo wakiangalia mitambo ya kiwanda cha matairi cha General Tyre jijini Arusha.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango (mwenye suti nyeusi) akioneshwa moja ya mashine zilizokuwa zinatumika kutengenezea matairi katika kiwanda cha General Tyre kilichopo katika jiji la Arusha na Mwangalizi wa Kiwanda hich, Bw. Leonald Mgoyo. Serikali ina mpango wa kukifufua kiwanda hicho baada ya kusimama uzalishaji tangu mwaka 2007.
Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Tume ya Mipango wakitazama bidhaa zilizokuwa zikitengenezwa na kiwanda cha matairi cha General Tyre. Serikali ina mpango wa kufufua kiwanda hicho ambacho kilisimama uzalishaji tangu mwaka 2007.
Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo na baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wakifurahia jambo wakati wa ukaguzi huo.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango (mwenye suti nyusi) akiagana na Mwangalizi wa Kiwanda hicho, Bw Leonald Mgoyo baada ya ukaguzi wa kiwanda hicho. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Bw. Gideon Nasari na kushoto kwake ni Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango anayesimamia Klasta ya Uzalishaji, Bw Maduka Kessy.
Picha na Joyce Mkinga,
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
OFISI YA RAIS, TUME YA MIPANGO
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad