MGOMO WA WANAFUNZI : POLISI WAZUIA WANAFUNZI WA LYAMUNGO KUELEKEA KWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


27 Mar 2014

MGOMO WA WANAFUNZI : POLISI WAZUIA WANAFUNZI WA LYAMUNGO KUELEKEA KWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro- Robert Boaz


Mwandishi wetu, Moshi

JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro, kikosi cha kutuliza ghasia (FFU)kimefanikiwa kuzima maandamano makubwa ya Wanafuzni ya Shule ya Sekondari Lyamungo, iliyoko wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro, uliokuwa ukielekea kwa Mkuu wa mkoa huo, Leonidas Gama.

 
Maandamano hayo yaliyotokana na kile kilichodaiwa kuwa ni baadhi ya wanafunzi kutoridhishwa na ratiba ya chakula shuleni hapo, yalilenga kufikisha ujumbe katika ofisi ya mkuu wa Mkoa, zilizoko mjini Moshi, kilomita zaidi ya 21 kutoka shuleni hapo.

 
Taarifa zilizothibitishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani hapo, Robert Boaz zinasema kuwa wanafunzi hao walianza chokochoko hizo juzi jioni baada ya ratiba ya chakula iliyokuwa ikionesha kuwa walitakiwa kula wali kubadilishwa ghafla na uongozi wa Shule bila ya kutoa taariofa kwa serikali ya wanafunzi.

 
Kamanda Boaz amesema wakiwa wameshafika eneo la njia panda Umbwe, maandamano hayo yalizuiwa na kikosi cha kukabiliana na ghasia (FFU) lakini akaendelea kusisitiza kuwa taarifa zilizotapakaa mitaani kuwa kulikuwa na hali ya kushambuliana kati ya FFU na Wanafunzi hao sio za kweli.

 
“Hakuna makabiliano, jeshi la polisi kikosiu cha FFU hakijafanya mashambulizi yoyote kama inavyodaiawa, kilichotokea pale ni kwamba baada ya kufika njia panda Umbwe, tulifanikiwa kuwahi na kuwazuia, hatuwezi kuruhusu watu kuandamana bila kufuata taratibu,” alisema Boaz.

 
Kamanda Boaz alisema kuwa taarifa kamili zitatolewa baadae ambapo ameongeza kuwa tayari uongozi wa wilaya, wakiwemo Afisa elimu sekondari na Mkurugenzi wa Halmashauri wameshafika shuleni hapo kuzungumza na Wanafunbzi hao kujua kiini cha maandamano hayo ni nini.

 
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Hai, Novatus Makunga, amesema kuwa lengo la maandamano yanawezekana hayakuwa mabaya lakinii utaratibu uliotumika sio sahihi.
 
 
“Ni kweli kulikuwa na maandamano ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Lyamungo, inawezekana walikuwa na nia njema tu, lakini naendelea kusisitiza kuwa utaratibu waliouchukua sio sahihi kisheria, hapa tunavyoongea hakuna taarifa au malalamiko yoyote yaliyofikishwa ofisini kwangu,” alisema Makunga.

 
Taarifa zilizopatikana na kuthibitishwa na uongozi wa wilaya ya hai kuwa hiyo sio mara ya kwanza kuwepo kwa tatizo kama hilo kwani Aprili mwaka huu wanafunzi waliripotiwa kugoma baada ya kutokukubaliana na mabadiliko ya ratiba ya chakula shuleni hapo.

 
Na Fadhili Athumani- Kijiwe Chetu Blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad