HABARI ZA KIMATAIFA :HEIFER INTERNATIONAL TANZANIA YAZINDUA MRADI MKUBWA WA KUENDELEZA SEKTA YA MAZIWA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


31 Mar 2014

HABARI ZA KIMATAIFA :HEIFER INTERNATIONAL TANZANIA YAZINDUA MRADI MKUBWA WA KUENDELEZA SEKTA YA MAZIWA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI


Naibu waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambae pia alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Mh Kaika Telele akiongea na wageni waalikwa na wadau wa sekta ya Maziwa Afrika Mashariki uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwl Nyerere Mwishoni mwa Wiki.
 Mkurugenzi Mkuu wa Heifer International Tanzania, Dk Henry Njakoi akiongea na wageni waalikwa na wadau wa sekta ya maziwa nchini na wa kimataifa waliofika katika uzinduzi wa Mradi wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki uliodhaminiwa na Mfuko wa Bill na Melinda, Mradi huo mkumbwa ulizinduliwa ijumaa iliyopita katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere uliopo Jijini Dar Es Salaam
 Mkurugenzi Mkuu wa East Africa Dairy Development (EADD), Mh Rakesh Kapoor akichangia mada kwenye uzinduzi wa Mradi wa Kuendeleza sekta ya Maziwa kwa Nchi za Afrika Mashariki mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere, jijini Dar Es Salaam. Mradi huo mkubwa kutoka Heifer International Tanzania umedhaminiwa na Mfuko wa Bill na Melinda Foundation
Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo ambae pia ni Naibu waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mh Kaika Telele akifungua Pazia kuashiria Mradi huo wa Kuendeleza sekta ya maziwa umezinduliwa rasmi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere uliopo jijini Dar Es Salaam.
 Mjasiliamali wa Maziwa kutoka Mkoani Iringa, Bi Diana akitoa Ushuhuda wake kwa wageni waalikwa kuhusu mafanikio aliyoyapata akiwa kama mdau wa sekta ya maziwa.
Mgeni Rasmi katika Uzinduzi huo ambae pia ni Naibu waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mh Kaika Telele akimpongeza Mjasiliamali wa Waziwa kutoka Mkoani Iringa, Bi Diana wakati wa uzinduzi wa Mradi wa kuendeleza Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki.
Mkurugenzi Mkuu wa Heifer International Tanzania, Dk Henry Njakoi akiongea na wageni waalikwa na wadau wa sekta ya maziwa nchini.
 Baadhi ya Wageni waalikwa na Wadau kutoka Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki wakifuatilia mada kwa makini wakati wa UZinduzi wa Mradi wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki
 Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ambae pia ni Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mh Kaika Telele akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Heifer International Tanzania na EADD pamoja na wadau wa Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki.
 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mh Kaika Telele ambae pia alikuwa mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Mradi Mkubwa wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya Kilolo mara baada ya kumalizika Uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere uliopo Jijini Dar Es Salaam Mwishoni mwa Wiki.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad